to the LPCA home page Archives of Popular Swahili logo

ISSN: 1570-0178

Volume 8 (25 October 2006)



to the APS home page



Ukumbusho

by
Dr. Achille Mutombo


address:
D-72124 Pliezhausen
Germany


 

 

Ukumbusho

 

Ukumbusho 1: ukumbusho ni nini?

Leo minta anza kwandika mawazo yangu na mambo ile iko ina nifikia uku ku Allemagne mu kiswahili. Mishina wa kwanza hapana. Zamani, nawaza kunapita miaka ata mia moya na bia mu njia, kulikuwaka muntu moya wa ku Zanzibar alifikaka umu mu Allemagne. Jina lake ilikuwaka ni Bin Amur nawaza. Balimuitaka juu ya kufundisha bazungu kiswahili ya kule Zanzibar. Sasa ule kijana ali andikaka bintu biote bile alikuwaka anaona mu mikini ile alipitshiakamo. Mina kumbuka asema mu Amsterdam alishindaka kulala, sababu alionaka ba bibi na ba bwana beko banatembeya mu njia benye kubambana ku mikono ao beko natwangana milomo pa ku lamukiyana. Ile mambo ya vile hayikukuwake kule Zanzibar hata. Njo pale alishikiyaka boka. Hakujuake asema eko fuashi kani. Ni bantu ya namna gani aba? Kiisha anonyesha mu ile kitabu yake namna alifikaka kule Berlin na vile bantu bali mupokeyaka. Kale ka kitabu ule kijana ali andikaka, kekwako na leo huyu mu ma bibliothèques ya bazungu. Kwetu haba kajue hapana. Lakini bantu mingi banazobeleya kusoma kale kenyewe ka kitabu mu ki allemand. Sababu muzungu moya wa ku Berlin njo ali ka traduiraka mu kia kwabo.

Mina ona barafiki bengine bale niko nabo uku ku bulaya, bana anza sasa kwandika mu kia kuabo. Bana isha kufunda masomo mingi ya bazungu, lakini pale bana anza kuzeka, bana anza kurudiya sa ku butoto vile. Ni kweli banasemka asema kuzeka ni kurudiya ku butoto. Njo kusema asema bana anza kukumbuka mambo ya zamani. Tena banapenda sasa kushikiya mpaka ma adisi ni mimbo ya pale bangari batoto. Ni ile mambo tulianzaka kushikiya mu ka mwimbo ka ku annoncer nako théâtre ya mufwankolo ku Lubumbashi: Ilikuwa zamani. Ningali mutoto. Ilikuwa zamani, ningali mutoto. Bibi Veronika. Funga bintu twende. Bibi Veronika. Funga bintu twende. Kwetu ku mugini. Inchi ya furaha. Haka ka mwimbo ka zamani kana onesha kama, kila muntu eko na mambo ile anakumbukaka. Ka mwimbo ya Mufwankolo kana onesha tena asema, hakuna muntu ataweza kuiishi pasipo kuwa na mawazo ile ina murudisha mbele ku mukongo. Ata mu tabia ya kwetu ya kuteka ma adisi, ili kuwa tena ni mpaka ile mawazo ya kukumbusha mambo ya zamani. Lakini ile ukumbusho aina juu ya muntu kubakiya tu sa mu ndoto vile hapana. Bantu bana kumbuka ao bana jikumbusha mambo juu ya kuona namna ya kwendelesha maisha. Kama muntu eko mpaka mu mambo ya zamani pasipo kujiuliza asema kule tuko tuna enda ni wapi, utashikiya bata muuliza kuko benjake asema: weye ungali mpaka unalota? Uta shutuka mashuwa ao courrier inaisha kwenda. Kazi yako. Lala paka vile. Uta shitukaka trop tard

Niko na barafiki mingi uku ku bulaya. Lakini mimi mwenyewe mina lala miaka mingi huku kwa benyewe. Shikuwajiyake hata. Njo vile mu la vie. Uta shikia tu leo moja ku ba rafiki ana kuandikia ka email asema : minatoka mukutuma ka kitabu ku imprimerie. Kama una uliza asema ni mambo kani ile anandika? Mbele ana anza kucheka. Kiisha anaongeza asema aliandika mu kiakuabo. Sasa namiye minasema asema: pahari ya kuendelesha mpaka na kuandika mu ma luga ya benyewe, bashi na miye ni andike sasa mu luga ile ni li komeya nayo. Mina kumbuka muzuri siku ile frère Mbwebwe arikufuaka. Ali patiaka malari ku Mbujimayi. Ali kimbiriyaka kule ku Kasai pale bitumba biri lamukaka ku Lubumbashi asema bakasai bende, banapita kuuji bantu. Kule ku Bakwanga frère Mbwebwe aliendaka kufuchama, ali anzaka ma kaji yake muzuri. Ali anzaka kuenda mu ma njia juu ya ku angalia batoto ya mu nsoko. Bamingi bali poteshaka bazazi yabo mu njia ya mashua pa ku kimbia mambo ya geopolitique ile ili lamukaka ku Katanga mu 1992. Bengine beko tu na bazazi yabo. Lakini beko bana basema asema beko na buloji. Njo kule mateso inafikishaka bantu. Nilishikiya asema, kunapita tu mienji tatu ao ine, kuko batoto ba mu nsoko ba ku Mbujimayi, bale baribatshoma. Bengine bari bapika tu maibwe bana kufua. Ile mambo ikaleta haya sana. Badiamantaires balisemaka asema, bale batoto bana kuyaka kuiba bintu yabo mu nsoko. Angalia mina tafuta na kusabu mambo inyewe ile nili anza kusema pa lufu lua Frère Mbwebwe. Eyo. Mina ona sasa kinyewe nili anza kusema. Pale alikuyaka mu hopitalo ku Belgique, ba munganga bali semaka asema hakuna namna ya ku mupasula tena. Ali kuwaka na ma boules mingi mu kichua. Njo mana ali kuwaka paralisé. Ile operation ili pashuaka kukawa ma sa mingi sana. Lakini aikuweza tena kumuponesha sababu ma metastases ili kuwa mingi sana mu kichua yake. Sasa siku yake ya muisho, njo kusema mbele ya ye kufa kwake, nili endaka kumuona ku opitalo. Ma soeur moya muzungu wa ba Soeurs de la foi ao ba Christ roi, mi shijue tena muzuri, njoo ule ali muletaka. Ule ma soeur ni infirmière kule ku CNPP ya Kinshasa. Alikuyaka eko anamuletea Frère Mbwebwe kommunio kila juma. Ma soeur mwuingine wa ku Mbujimayi, jina lake ni Odile Mbuya, ali muchungaka Frère Mbwebwe muzuri sana. Sasa ile bushiku bua muisho, nili endaka kumuona Frère, tuli anzaka kusala naye. Hakukuake tena na namna ya kusema. Lakini ali kuaka anafuata na kusikia tu biote. Kama mina imba muimbo ya mu francais utaona tu anendelesha kulala. Lakini uki imba muibo ya mu kiswahili kia ku Lubumbashi, unaona vile ana anza kukuangalia na ku réagir. Njoo kusema asema: ni ile luga yako ya kuanza ile ulianzaka kusema pa butoto njoo ile ita rudia mbele ya kufua kuako. Kumbe ni bia kweri bile banasemaka: kubuzee njoo kurudia kubutoto. Una anza kupenda baku bembelesheko na kukutapa sa mutoto. Kama muntu ye apana kukulamukia, unawaza asema ana kupunika ao anakuchukia. Njoo mambo ya buzee vile ina ikalaka. Ni paka mambo ya zamani njoo ile unapenda kusungumuza na kucheka. Bia sasa biote una anza kuona asema ni bia bule. Ba Kasai bana semaka asema: malu a chanana mon frère wanyi. Tena ina kuyaka nguvu pa kubibamba bile bintu bia sasa bibakie mu kichua. Paka bia zamani njoo bile biko bina rudia. Pa butoto tulianzaka kuimba ka mwuimbo kamoya ka ncheko sana. Tu li anzaka kuimba asema:

Buzee yolele. Buzee yo. Buzee yolele. Buzee yo. Nalala mulango wazi buzee yo. Nalala mulango wazi buzee yoo. Ni ki kumbuka buze si lale. Ni ki kumbuka buzee silale. Nalala mulango wazi buzee yo. Nalala mulango wazi buzee yo.

Lakini apa mina anza kuandika mu kiswahili yetu ya Lubumbashi, ni juu ya kusema asema njoo luga ile tulikomeya nayo. Njo kia kwetu. Bantu bamingi habajue asema ile kiswahili ya Lubumbashi ilitokaka wapi. Kama unangalia muzuri, utaona asema ile mikini yote iko mpembeni ya Lubumbahi, haisemake kiswahili. Bantu ba ile mikini beko banasumbulia mu kilamba, ki kaonde, kisanga, kibemba, kizela, kilala. Kiswahili kia Lubumbashi kili anzaka mu ma 1915. Mwaka kesho njo Unionminyere ita enesha miaka mia moja. Ile kiswahili ya Lubumbashi kilianjia mu ma componi ya Unionmnyere. Mule bantu bote bali kuwa benye kuchanga changa ma kabila ya kuachana. Muli kuwaka ba Kasayi, ka Kabinda, Banyasaland, ba Karunda, Bakachokwe, Balubakat, Babemba, Balamba...Sasa bale bantu bote baliwezaka kusumgumuza njee? Francais na ki flamand hababifundake tu leo na kesho. Tena mu Lubumbashi muinyewe bantu balikuwaka banasungumuza mu ki Fanagalo. Njo vile baba Anna, mwalimu Johannes Fabian ali ni elezeya. Ile luga inaisha kupoteya. Ilikuwa luga ya ba nyasaalandboy. Aba ba nyasalandboy ni bale bali ingishaka njanja mu katanga mu 1910. Sasa bazungu bali ingishaka ile luga ya kiswahili mu Katanga juu ya bantu bashi anze kusilizana na bantu ya mu Rodésie. Ilipaswaka kuleta luga moya ingine tu. Luga ya kutoka mbali. Sasa ile luga ya kiswahili bantu bo benyewe balikuyaka kuyitengeneza kati yabo. Njo mana uko na ma mots ya mu Tshiluba, kibemba, kisanga....mu kiswahili kia Lubumbashi.

Zamani tuli anzaka kushikia haya pa kusema kiswahili kia Lubumbashi. Bantu ya ku Kongolo, Kalemie na Maniema balikuyaka beko bana tucheka saana. Ata mu ma misa, tulikuwaka tunasema kiswahili bora, kiswahili safi. Pakusema asema muntu anani chambula, tulikuwa tunasema asema muntu ananizarau. Pakusema asema mina itshika na ku confirmer asema ule muntu anasema bia kweri, tulikuwa tuna geuza asema nina hakikisha. Pakusema asema nilisoma mu journal, tulikuwa tunasema asema tulisoma pale ma gazetti. Kiswahili kia kweri kilikuwa tu ni kile kia Kongolo, Kalemie, Maniema ao Tanzania. Sasa siku moya ku likuwaka mwalimu moya wa ku université ali pitaka ku television. Jina yake ni Takizala. Mukubua yake ali kuwaka kometa njo kusema mu francais Commissaire d'état. Mbele ya kupita kwake ku télévision, tulijuaka asema wakati moya ivi, ule mwalimu wa ku Université ya Lubumbahi ali fwanyaka conférence ku Kinshasa mu 1978 mu kia kuabo. Yeye ni mwenye kujuwa kikongo muzuri. Alisemaka biote mu kikongo. Bantu bengine bali traduiraka mu francais na mu angele. Ali pendaka kuonyesha kama kuko namna ya kusema mambo ya akili ya yulu kabisa mu ma luga yetu ya bantu beushi. Siku ile alipitaka ku television ya Lubumbashi, ilikuwaka ni juu ya kusema asema inapashua kuitshika asema kiswahili ya Lubumbashi nakio ni kiswahili. Ata kama kina achana na kile kia Kongolo, Kalemie, Maniema na Tanzania ...ni luga nayo ile bantu beko nashikiya. Nayo ni luga mule bantu beko banafanya ma expériences yabo. Mushinikate mbele karimi. Minta rudiya ku hiyi mambo. Mishita sabu hapana. Mina juwa muzungu moja eko huku ku bulaya. Alikuwaka père. Ule bibi beko naye, balipatanaka naye mpaka mule mu bu père. Yeye alikuyaka masoeur. Sa vile balipatanaka beko bana sema Ciluba. Na leo huyu, beko tu nasema ciluba. Zaidi kama kuko mambo ya mateso munene ao mambo ya furaha munene. Kama kuko mambo ile ina angaliya roho, ao mambo ya ma ncheko ya bien bien, pale ni mu ciluba tu. Ilikuwa tu ni ka mufano juu ya ku mu appuyer ule mwalimu Takizala. Turudiye sasa ku ile emission ya télévision. Ile shiku kuli tokaka bubishi mingi sana. Bamingi asema: kiswahili kia kweri ni kiswahili safi kile kiko na sarufi. Sasa ibi bia mu Lubumbashi kila muntu eko ana sema vile ana oneyamo. Ni kusema tu kisemeseme. Mule bita endeya, njo mo.

Ni kweli, ile kiswahili ya Tanzanie kina ikalaka butamu pakukishikia. Hata aushikie mambo inyewe beko nasema, lakini tu ni butamu ya vile ma mot iko inatoka. Tulikuwaka tuko nasema asema: bale bantu banajuwa kuporomosha Ukiona muzuri, bote bale balikuwaka beko banasema ku radio oa television, balikuwaka bantu ya kule balianzaka kusema kiswahili ya sarufi. Leo, shiye luetu hatuna tena na complexe. Mu misa tunasemaka namna ingine. Lakini mu njia, tukotunasema tena namna ingine. Kua mufano: kuli kuwaka Monsieur l'Abbé moya ivi jina lake Kasongo. Ali kuwaka mu Gécamines. Tena balianzaka kumuita asema Mukulu Kasongo. Rafiki yake moya naye Monsieur l'Abbé alikufaka. Jina yake alikuwaka Mukulu Mwamba. Bali patanaka wakati moya tena na mwuingine Monsieur l'Abbé, jina yake Alimasi. Bali anzaka naye kumwuita asema Mukulu Alimasi. Bote tatu bali ingiyaka mu mambo ya sala sana. Mukulu Kasongo alikuwaka eko na kokota bantu mu Notre Dame de la Paix. Bantu bali chanjaka namna ya kusema. Bana kuya na biswahili bia namna ingine. Pakulamukiyana ilikuwaka asema: Wa Bwana yambo. Wa malaika yambo. Uli enda mu njangua? Ulisikia mafundisho ya mutumishi? Tena ma mimbo ya mu jangua, ilikuyaka yote mpaka ya mu kiswahili yabo. Kile kiswahili hakikuyake tu bora kabisa. Kilikuyaka ni kiswahili kiabo. Na mu namna ya kusema mambo, ili onekanaka tu asema, kama muntu anaendaka mu jangua eko anasema namna yake. Mambo ya Mungu bantu bali anzaka kuyisema mu luga ya mu jangua. Sa vile ile mafundisho ili kuyaka kuingia sana mu maisha ya bantu, na namna ya kusungumuza mambo ingine ika anza nayo ku changer. Lakini nilionaka asema kama bantu banapenda kuikala pashipo ma tension, kuikala tu ivi, beko bana cheka, ilikuwa ni mu kiswahili yetu ya mu nsoko tu. Mule njoo mulikuwa mambo ya kuchangamusha nayo bantu. Hiyi ingine ilkuwaka na ma sérieux mingi. Bashi mu mafundisho ya Mukulu Kasongo hamukukuyake mambo ya ncheko ata. Kama Père anasema kiswahili ya ba wayambard, bantu balikuyaka banacheka tena banafurayi sana.

Kua kifupi, tuseme asema, kiswahili ya Lubumbashi njoo kile tulikomea nakio. Ata muko ma mots ya francais mingi, njoo mpaka vile. Tunajua asema muko na na mots ya mu ki kasai, ya ku ki kabinda, ya mu kibemba, ya mu kifanagalo...Ile luga ni ya changachanga sa manguwo ma mu nkombo. Mu mufuko moya muko tuputula, ma nsumishi, tulenso, masengele, ma pantalon, ma jipe, mabluze... Ni juu bantu benyewe bale beko mu Lubumbashi, bantu benyewe bale bali jengaka hiyi mukini, ni ba ku changa changa tu. Mambo ya pili, ni ya kusema kama hatuwezi kuwa na complexe hata. Kiswahili kinyewe kia Tanzania shi ni kia ku changa changa na ki arabe, na ma mots ya mu ma luga ya bantu beushi ba kule ku ngambo ya ocean indien. Sasa complexe ni ya nini? Njo pale mishi one tu mambo yenyewe ya kuleta complexe. Hata mambo ya akili ya kabisa, ya yulu kabisa, unaweza tu kuyi andika na kuyi waza mu kile kiswahili kietu kia Lubumbashi. Angaliya : kuko philosophe moya wa ku Vienne, jina yake ni Karl Popper, alisemaka asema, inapashua kuandika bintu biote peupe, juu ya bantu bote bakushikiye. Kama unaisha kushikiya kintu muzuri mu kichua yako, utaweza tu kupima kukieleza mu luga ile batoto na ba mama beko bana shikiya. Complexe na haya ni bintu ya ovio kabisa.

Ukumbusho 2: ba bwana ncheko

Kuko ma jina moya hivi, kama una ishikiya bana itaya, utaanza tu kucheka we mwenyewe. Ile siku, rafiki yangu moja ali nitumia cassette vidéo ya ba Mufwankolo Mwana wa Lesa. Mina shangaa sana. Minasema asema: kumbe uyu baba angaliki tu ana cheza théâtre? Haya achaka kote kule. Pa butoto tulikuwaka tunapenda kushikiya kale ka mwimbo kakusema:

Ilikuwa zamani/. Ni ngali mutoto/. Ilikuwa zamani /Ni ngali mutato./
Bibi Veronika/ funga bintu twende/Bibi Veronika/funga bintu twende/
Kwetu ku mugini/inchi ya fruraha/kwetu ku mugini/Inchi ya furaha/

Ule baba Mufwankolo mwana wa Lesa, alikuwaka na fujo mu ma théâtre yake sana Kama unamuona mu njia, eko tu muntu wa bupole bupole. Sasa, waza mbele kama unakutana naye mu njia, muntu ana kuelezea asema ule njo mwana wa Lesa. Hata kama haseme kintu, we mwinyewe una anza tu kudichekeya. Uta anza kukumbuka bintu anasemaka ao anafanyaka mu théâtre. Pa ile foto niliona ya nkundi ya Mufwankolo bote banaisha kuzeka. Sasa kuko mwuinyewe ule eko anabakiya kiyana? Hakuna. Shi bote tuko tu mu njia. Njo vile rafiki mwuingine ali ni elezeyaka asema, alikuwaka mu njia eko napita luake tu. Anaona batoto beko banacheza futubolo. Angalia sasa katoto kamoya katoke tu kule, kamufuate asema:papa Kalonji yambo. Hakusemaka kintu. Akapita tu mu bu Kabeya Sotshio. Njo kusema : anapika Serieux ya mbuzi. Unajua asema: Mbuji ye luake hachekake. Imbua shi ana oneshakako na furaha. Utaona anatenkeshako mukila. Lakini mbuji ye luake ni kupita tu eko anaria: mee, mee...Njo vile kuko bantu banaletaka tu ncheko bobenyewe pasipo kusema kintu. Kuli kuwaka tena muntu moya beko bana muita asema docteur Mundo. Alikuwaka na fujo mu ma commentaires yake saaana na zaidi. Kama ana anza apa, shi utalala na ncheko, mbavu inakuvundjika. Siku moya, alipitaka ku television. Ni ile wakati Reagan alikuyaka Président wa ku Amerike. Sasa yeye Mundo analanda asema Reagan alifikaka mu Lubumbahi juu ya malari. Ba Docteurs bote ba mu reánimation, ba Tshowa bana mushinda Reagan. Njoo bana muita sasa Dr Mundo. Ile saa anafika mu réanimation ya Gécamines, anaona vile Reagan eko anaria sana. Dr Mundo ana muuliza : Reagan ni mambo kani hivi ? Reagan anajimbu mu angele asema: I am pleuring. Pale Dr Mundo anasema vile, tulikufuaka mu ncheko sana.

Njoo vile inaikalaka mu ma fuashi yote. Hamukosake ba komédien ba kuanza kuleta ncheko. Mu Ruashi bantu bali anzaka kucheka mukubwa moya hivi. Jina yake ilikuwaka ni Muyambo. Ule mukubwa alipendaka kulambula milomo yake saana. Kama muko muna sumburiya, utaona vile eko analambula milomo mbele ya ye kusema kintu. Milomo inyewe inaisha kuya rouge kabisa sa tu alikakala kapenta. Ukione muntu wa vile mu njia, njoo una anza tu kucheka habaya kuelezea hata kintu.

Ukumbusho 3: mambo ya mu ma opitalo

Minashikiya asema ma opitalo ya kwetu haina tena vile ilikuwaka zamani. Zamani, tuli anzaka kuenda ku opitalo, tuna juwa asema, bata kupatia dawa. Sasa uko una enda, weye njoo wa kuleta dawa we mwuinyewe. Na pa kukupasula, ni weye njoo wa kuleta ma gants na ma nkamba ya kushona nayo kilonda. Bantu beko na kufa na ma malari ya bule bule tu. Utashikiya tu asema muntu alikufa juu ya malaria, ao typhoide ao grippe. Ni zaidi hiyi ma malari tatu tu, njoo iko inabeba bantu. Banduku, tuna fikiya wapi leo? Bobale beko banapenda cheo, lakini leo huyu banashinda kuendelesha mukini juu ya mambo ya ovyo ovyo tu. Zamani bantu balikuwaka banatoka ku Afrique du sud ao ku Rhodésie juu ya kuya kujitunzisha mu Elisabethville. Tena mukini inyewe ya Elisabethville, ilikuwaka muzuri sana. Ilikuwaka propre kabisa. Waza mbele vile Monsieur Wangermée alijengeshaka ile mukini. Ma njia yote ya mu ville, ilikuwaka saa jeu de dame. Ilikuwaka na ma michi ku mpembeni ya kila balabala. Na parc ya pale karibu na Institut Marie José na Collège Saint Francois de Sales, ilikuwaka iko inaletako ka mpepo kazuri. Leo huyu mina shikiya asema mule mu parc moote, munayisha kuyala ma nyumba ya bantu. Na ba nyama ba mu zoo, habanamo tena. Bia kurisha bantu binakosa, mpaka bia kurisha ba nyama njoo bita onekana? Nyama sa nsimba ao nchui, eko anakulaka mpaka ma minofu munene munene. Mukini ina haribika. Ntanda yafwa. Bantu bana konda sana. Ku ma masomo kunaingiya milomo. Pa ku passer, mpaka unatenkako mbele. Kama haupende kutenka, mwalimu atakula je? Ku ma masomo ingine, minashikiya asema mwaka hayijaisha, lakini palmarès inayisha kutoka. Mu ingine ma ville ya kule kwetu, sa ku Mbujimayi hakuikalake ko ma palmarès. Ni kusema tu asema: momote mule bita endeya, njo mo.

Turudiye ku mambo ya ma opitalo. Kulikuwaka Docteur moya wa makari sana. Jina yake alikuwaka Dr Rock. Bantu asema: kama tu anakupasula, lakini haufwate bile anakuelezea, ujue asema anaweza kukutukuna kile ki bandage kiote kiko pa kilonda mbele ya bantu. Biki kuume ata abi kuume, etali kaka yo moko, ni kaji yako. Mwingine Docteur alipendaka ku opérer eko nakawa saana. Ule Dr, ba infirmières haba kupendake zaidi kutumika naye. Juu tu ya ka appendicite aka, muko munakawa ma saa tatu ao ine mu salle dop. Asema kama tu infirmière ana mu elezeya asema, tufanyeko bupeshi, uta shikiya vile atakujibu : Ma fille, c'est moi qui opère et non pas toi. Bengine ba Docteur habakupendake kuandikiana dawa. Uta fika kuake, eko anakuelezea asema : kudia nsombe mingi. Utaona ile malari itaisha. Ba Docteur ba vile, bantu habakupendake kuenda kuabo hata. Uta shikiya tu ma commentaires ya bantu asema : ule ni Docteur mubaya sana. Eko na buimi sana. Pa ku kuandikiya dawa, mpaka kama anakujua. Kama hauna ndugu yake, kama uko muntu wa bule tu hivi, hata kuandikia dawa hata. Bengine na bo asema, mu réanimation njoo mulikuwaka tu sa mu missa. Kama muntu anona lufu lunakuya karibu, shi utashikiya tu mambo ata anza kusema pashipo bantu ku muuliza. Inaikalaka tu sa ni maungamo ya kweri kweri. bantu banafanyaka mule. Muntu wa heshima, wa ma abacost kila shiku, eko anaria mule tu sa mutoto kiloko. Eh. Njo vile. Ku malari hakuikalake mukubwa, hakuikalake mutoto. Kwenye kwa mambo zaidi, ilikuwaka ni kule ku ba majimu. Hawutaweza kuingiyako juu ya kuona muntu. Alafu kama bote bale beko mule, majimu ina balamuka, bana anza kukupika, uta kimbiliya wapi? Tulikuwaka na rafiki moya mu Lubumbashi. Nduku yake alikuwaka sa na ka majimu vile. Kale kamajimu kali anzaka kumulamuka wakati moja moja Kama bina kuya vile, uta ona anaenda kuifungiya mu nyumba. Siku moja, minaendako na ule rafiki. Nilisemaka asema, ni muone na ni mulamukiye. Kufika kule kuake, tuna kokola weee, yepana kujibu. Njo tunaanza kuita sasa na sauti ya nguvu. Kumwuisho ana jibu. Ana uliza asema: muna tafuta nini? Tuna muelezeya asema: tuna kuya kukuona na kukulamukiya Tunashikiya tu vile analamuka mu kitanda. Anachofeya kule ku mulango. Kiisha anafungula fenetre tu kiloko. Ana tosha mukono yake. Lakini hatukuona nsula yake. Ile saa minamupa mukono ana i tenkesha anatema: jambo sana. Kiisha anakokota mukono yake. Anafunga dikalashi. Kunaisha. Tuna muita tena. Anasema: shi mulikuya juu ya kunilamukiya? Eh!Shi mambo inaisha sasa. Pakutoka kule tunasema: kumbe hiyi majimu ni ya bia kweri

Ukumbusho 4: ma buzave ya jana na ya leo

Kama unashikia leo batoto ya masomo beko bana sema francais, shi uta shangaa. Muntu eko na diplome mumufuko, lakini eko anafanya ma fautes ya mingi sana. Una anza kujiuliza kama balifundaka masomo ya kweli. Na ku radio, na ku television, uko tu unashikia ma fautes ile bantu beko bana fanya. Pa zamani, kulikuwaka ba journalistes balijuwaka kuporomosha buzave. Balikyaka beko banacheza francais saa futubolo. Kulikuwaka bantu sa ba Kibambi Shintua wa Muselemba. Wakati moja hivi, yeye njo alikuwaka eko anasema mambo ya Président yote. Ilikuwaka ni buzave pa buzave. Francais ya kwerikweri. Mbele yake kulikuwaka journaliste muingine. Jina yake ilikuwaka Kasonga Mbunga Kalala Kafumba. Chefu ao sultani wa mumukini yabo, alikuwaka Kalala Kafumba. Kama naye alikuwaka wa mu famille ya bu sultani, atujuwe. Tunajua asema, bantu ba mingi banajipelekaka ku bu sultani bo benyewe tu. Kulikuwaka tena Dimanja Wembi, Kasongo Mwema Yamba Yamba, Kalasa Msiri, Kudura Kasongo, Tshimpumpu wa Tshimpumpu, Kabala Mwana Mbuyi, Atufuka Mbuze. Ku ba mama kulikuwaka Kabangu Ntshita, Mbungu Tshibangu, Sakombi. Aba bote, balijuwaka luga ya bazungu saana. Kudura Kasongo alipendaka kufanya bilan ya mwaka mujima mu le 31 décembre. Utamuona anatokeleya mbele na abacost ya new. Ata ikala pa ka tabouret kalefu. Njoo ana anza sasa kutelemusha bia kutelemusha.
Francais ya hiyi miaka, inaisha ku haribika sana. Tena bantu benyewe beko bana andika na ma fautes ya mingi sana. Njo vile mukini ina aribikaka. Kama bantu bana kuya kila muntu eko anasema na kuandíka vile anaona ao vile anapenda, njo mwanzo ya matelo ile. Sasa tuko tunaona tutoto tua mingi tuko tuna sema francais ku mulango. Zamani francais ili kuyaka ni ku masomo tu. Sasa batoto bana jua asema kama bana kuita ku telefone, inapashwa kujibu mu francais. Ku bulaya huku tuko, kuko bantu beushi mingi bale beko na complexe. Beko mpaka na ma francais mu kinywa saa yote. Sasa batoto yabo, bana zobeleya mpaka ma luga ya bageni. Bana kuya tu sa bazungu benye kujuwa ni luga moya tu. Kichua nakio kiko tu na fuashi juu ya kuweka ma luga mingi. Ni bantu beko na complexe ya kuwaza asema, ma luga ya kuheshimiya ni mpaka ile ya bazungu. Pale mufuankolo ana fanyaka ma theâtre yake haikalake ye luake na ma complexe. Shi eko anatutula kiswahili tu pashipo kikunkumina. Ku Kamerun, njo banashinda kuweka hata luga moja ya bantu beushi yanze kupita ku radio ao ku television. Ukiseme asema, babebe luga fulani, bengine batashirika. Njo bote banabakia sasa mpaka mu francais ya kuchangana kama na ma mots ya ma kabila ingine. Hata mu njia ya ku Kamerun, uta kutanisha bantu, na ba mama ba miaka mingi na invu kukichua, beko tu na ma francais francais ya kia kwabo mu kinywa. Kwetu ku Kongo kukwako bien. Tuko tunashikiya Kiswahili, Tshiluba, Kikongo na Lingala mu radio na mu television. Au moins tukuako na ma luga ya bantu beushi. Habina sa bia ku Kamerun.

Ukumbusho 5: musemeyo ya ba vijana

Mishi juwe kama bantu beko nasema leo namna gani. Kiswahili iki minachunga na leo ni mpaka kile tulikuya tunasema pale ningali ku Lubumbashi. Angalia francais ya bantu ya ku Kanada. Ina bakiya mpaka vile bantu balikuwaka banasema pale bariendaka ku ile mukini ya ba indiens, bana acha mukini yabo ya mu bulaya. Leo uyu, paweye kuona tu indiens mu ile mikini, inaisha kuya nguvu kabisa. Bazungu bali bauwa ba indiens sana. Lakini bekwako. Lakini si ba mingi zaidi. Mina shikiya asema, bazungu bale beko kule beko tu sa na kintu kiko kina bauma ku roho pa kuona bale ba indiens. Njo mana, beko na haya. Bana bapatia ba indiens tu biote. Ba indiens nabo habaone hata kia kufanya na bile biote banabapatia. Njo kuingia mu lutuku sasa. Bashi kama unapata biote haubitumikie, shi utakuwa sasa muvivu saana. Shi pamoya na mutoto ule muko munarisha buyi, hata anaisha kuwa na meno ya ku kata nayo tu ma minofu ao kuvinya tu ma nkalanga. Meno ya ule mutoto na mbanga yake habitakuwa na nguvu hata. Hatakuwa tu ana ongojea asema baba yake ao mama yake bamupatie biote.
Sasa kule ku Kanada, kuko ma mots ingine ya mu francais ya zamani sana. Lunga inaendeleya njo tu mu ngambo ingine. Njo pale mishi jue muzuri kama mambo yote ile niko na taya na ku raconter mu iyi mistari, ni vile bantu beko banasema leo mu Lubumbashi. Kuko tu ma mifano mingi ya nginsi bantu balikuwa banasema. Lakini hiyi sasa ni luga ya ba vijana, ya ba jeunes pour jeunes. Payari ya kusema tumbako, bengine balikuwa banasema shimbok. Payari ya kusema kuria bukari, bengine balikuwa banasema kudamer. Payari ya kusema kukata muntu milomo ao kutengeneza mambo bila kufwata vile réglements ao kanuni inasema, bengine balikuwa banasema asema inapashwa tusungumuze muzuri. Payari ya kusema asema bana mutosha damu mu mpwa, bengine balikuwa banasema asema bana mutosha bilomposhi. Payari ya kusema asema bana anza kucheza futubolo, bengine balikuwa banasema asema, bana selula. Futubolo inyewe bengine balikuwa banaiita asema bulundu. Lakini kama aina ya mpepo balikuwa bana iita tu asema kifumpa. Kifumpa njo ki futubolo kia ma papiers na ma nguo yenye kufunga na nkamba. Ki bulundu njo kile ki futubolo kia bazungu. Ki bulundu kiko kia mupila tena kiko na mpepo ndani. Sasa payari ya kusema asema tuna cheza futubolo, bengine balikuwa banasema asema banacheza kabumbu Mukucheza kabumbu mwinyewe kama unapenda mwejako akupatie ao aku passer futubolo, bengine balikuwa banasema asema inapashwa amurivite futubolo. Njo maana, ata kama muko ku meza, muko munakula ao muko munakunywa, bengine balikuwa banasema asema inapaswa babariviteko mbele munofu ya nyama. Sasa kama muntu eko ana kawa sana na futubolo, anapenda kuonesha vile anajua kuchola benjake, balikuwa banasema asema eko na maweti. Ata mu kusumbulia tu mambo ingine, kama unaona muntu eko anakawa mbele ya yeye kufanya kintu, unaweza kusema asema, eko na maweti sana. Lakini kama muntu hakawake na kukamata ma décisions, na kupita kubitendo mara moja, balikuwaka banasema kama ule muntu hana weti hata. Kama sasa muntu eko na bulale luake. Kama eko anafanya mambo yote paka polepole, bana weza kusema asema eko analenga sana. Eko analengama sawa bukari ya kimbala. Ata ma lampi ilikuwa ya kuachana. Katoritori njo ile lampi ya nchupa banaisha kuwekamo pétrole na lukamba luko lunawaka. Hiyi ingine ilikuwa ni ma lampi ya pétrole ao ma ampoules ya courant. Payari ya kusema asema tuko tunakunywa mpombe, bengine balikuwa banasema asema beko banatelemusha. Ile wakati njala ili ingiyaka sana, bantu bali kuwa banasema asema tunaisha kuonana, njo kusema tunaisha kula bukari. Lutuku ilipata njina ingine. Bengine asema ni cint cent, bengine asema ni Chorse. Bengine na bo asema ni chichampa.

Ukumbusho 6: ma bunga

Leo njala inaisha kuingia mu mukini sana. Zamani, bantu balikuwaka banakula mara mbili kushiku. Kulikuwaka bukari bua midi na bukari bua mangaribi. Bale balikuwaka na ma moyens, balikuwaka banakunya chayi asubui na kuriako ata ka kistolet. Kama muko na franga kwenu, kale ka kistolet bana kapakalako ata manteka ao bleuband. Lakini kama bile biote habinako, utaweza kuisha njala ya asubui na ka kimbala. Kimbala ni bukari bule buli lala. Ku ma ngambo ingine ya mukini yetu ya Zaire, sa ku Kasayi, balizobeleyaka kula kimbala sana. Sasa ma bunga nayo ilikuwa yakuachana. Kuli kuwa bunga ya moko na bunga ya nchenge. Bengine asema ni bunga ya mulobelo ao bunga ya muindi. Lakini kama muntu eko anasema mambo ya ovyo, kama hakuna kia kabaila kiko natoka mu kinywa yake, banaweza kusema asema, ni ma nchenge tu ile eko natosha. Hakuna kia kintu. Minashikia asema ku ngambo ya Kinshasa na Bandundu na Kananga banapenda kula bunga ya moko. Ngambo ya Mbujimayi na Katanga njoo bana kula zaidi bunga ya moko na ya mulobelo yenye kuchanga. Ku ma pori kule nilikuwaka ni nanenda, sa ma ngambo ya Kansenia bantu balikuwaka banakula bukari na malaki. Lakini mu ville malaki ao muchele hayikukuwa chakula ya kueneya muntu anasema asema anaisha kula hapana. Kama unamuliza muntu kama anaisha kula, ni kusema unauliza kama anaisha kula bukari. Muchele ao bilashi ao malaki ni ya kuongezeya po tu sa siku ya feti. Kula kua kweli ni kula bukari.
Alafu ma mboka ilikuwa namna gani? Nyama njo ilikuwa mboka muzuri kupita yote. Pa butoto tulikuwaka tuanimba asema : Bukari na nsombe mama, shi butake. Bukari na nyama mama njo pa lufu. Kulikuwaka tena namna ya kuimba asema Bukari na nsombe mama shi butake. Bukari na nkuku mama njo pa lufu. Nkuku ilikuwaka ni mashiku ya feti njoo munauwa nkuku. Siku ya bonane ni shiku ya kula nkuku. Siku ya noele nayo ni shiku ya kula nkuku. Ao kama kuko mambo ingine munene. Kama mugeni anafika, bata muuwiya nkuku juu ya kumupatia heshima na kuonesha kama bana mupatia poids mingi. Mugeni akifike bana mupatiya tu nsombe ya kuchacha, njo kusema bana muona tu bule. Ana kuya tu ni muntu simple, muntu wa ovyo. Kama ni nkuku wa buko inapashwa bipande yake biote biko mule mu kiungu. Na ma mikulu yake bata ifunga na ma intestins ya nkuku. Na kichua ya nkuku kinyewe utakikutana mpaka mule mu kiungu. Ni paka milomo ya nkuku na manyonya na mankucha njo itakosa. Tena muko mwenyewe, anapashwa kufunga bile biote bitabakiya ju ya kuenda kubikuria kwake. Kuko mashiku ingine kama mambo iko munene sana, banaweza kuchinja mbuzi.

Ukumusho 7 : ma samaki

Leo tuta pima mbele kukumbuka ma mboka ingine tulikuwa tunakuria nayo bukari. Ku masamaki kulikuwa makoki ya Lualaba, kabambale, ndakala, tundakala, milonge, bitoyo, tilapia. Tutajikaza siku ingine, kama tuko na sa mingi, juu ya ku décrire kila samaki vile eko. Mpaka hiyi miaka ya muisho, njoo bantu bana anza kulia poisson de mer, ile beko bana ita asema la mer ao thomson. Jina inyewe ya Thomson kama ita tokeya wapi, miye na weye atujue.

Ukumbusho 8 : ma samaki ingine

Mishijue kama kuko ma samaki ingine ile mishijue majina yayo. Ku ngambo ya Kinshasa kuko samaki moja hivi bana itaka asema nina. Ule samaki eko na courant mu mwili yake. Kama munabumbana naye mu mayi, utashikiya wemoya vile electricité itakupita mu mwili. Kulikuwaka muimbo moya ya ba zaiko, beko na imba asema nina alengisaka, njo kusema nina anatetemekaka. Sala vile mishikuishi zaidi ma ngambo ingine ya mukini kule kuko mitoni mingi, shitaweza kutaja majina ya masamaki ya kuachana. Na kazi inyewe ninilakaka ya kuandika vile kila samaki eko ku nsula, ku mukila, ku miba, ku milomo, kubunene, ku munofu kuinyewe..ni kazi iko nguvu sana.

Kulikuwaka baba moja wa ku inchi ya Mali. Jina lake alikuwa Hammadu Hampaté Mba. Njo fuashi inyewe akili ilikuwa yenye kupumujikiya tu kimwa. Alijua mambo mingi saana. Alijua mambo ya bazungu na mambo ya bantu beushi. Luga ya Francais alijuayo muzuri, sababu alikuwa anaandika mu ile luga ma bitabu yake. Alijua mambo ya michi, ya banyama, ya ba ndeke, ya ba nyoka, ya matunda, ya mauwa..ya mukini yake muzuri kabisa. Biote bile bilionekana asema ni mwenye ku bijua pa roho tu. Eko kama ananza kubisema hapa, bilikuwa binatelemuka tu kama mutoni ya Lualaba. Tena, alijua adisi ya bantu beushi na zaidi, adisi ya bantu ya kabila yake sana na zaidi. Sasa ile kabila yake ilikuwa ya bantu beko sa yote mpaka mu njiya. Njo mana ba peuls ao fulani beko mu ma inchi mingi ya ngambo ya afrique de l'ouest, Afrika ya mangaribi. Hampaté Mba alikuwa muzulumani. Ba muzulumani balijuwaka kusoma kupita ba Kristu, sababu balikuwaka banapata mara moja ile kitabu kia bitabu bana ita Koran. Ile kitabu kia bitabu kama kiko mu nyumba yako, haipashwe kukuye kitabu kingine kienye kulalapo. Yulu ya kile kitabu kia bitabu, hakupashwe kuya kitabu kingine. Ni ile namna banaheshimiya kile kitabu kia bitabu. Tena mambo yenyewe kuandikwa mule ndani, habaletake nayo bubishi. Benyewe ma bubishi pa mambo ya mungu zaidi ni bazungu. Njo pale bakristu mingi banaikalaka mpaka mumabubishi ya kila namna. Ba muzulumani balikuwaka na ma masomo ya yulu sana mu ma miaka 1000. Kua mufano bantu ba ku ma Université banapenda sana kutaya université ya Timbuktu kule ku Mali. Kulikuwa bantu benye kuandika bitabu mingi. Tutarudiyaka pa ile mambo ya Timbuktu siku ingine. Nilipenda tu kusema kama, kuna ginsi ya kujua mambo ya mikini yetu ya bantu beushi tena na kujuwa mambo ya bazungu muzuri kabisa. Sasa kuko bengine banapenda bo kufanya buzungu mu mambo yote. Banakuya tu sa banashikiya haya ya kujionesha asema ni bantu beushi. Tena batoto yabo habajuwe ma luga ya bantu beushi. Sasa ile maluga beko bana sema ni ya ba nkamboyabo? Hampaté Mba aliandika tena na alfabe yake tu juu ya kuandika luga ya ba fulani. Aliandika adisi mujima ya ba Fulani, na kule balitoka. Bengine bantu ba kule kuabo banasema asema ile alfabe ina fanana sana na ile ya barabu. Bangependa a inventer alfabe ya bantu beushi bila kuchanga na madamu ya kutoka ngambo ingine. Sababu mu Afrika kulikuwaka ma alfabe kiloko sana. Mpaka ngambo ya ba ethiopiens, ku Kamerun na ku Liberia. Hiyi ma inchi ingine ilikuwa tu mu bushiku. Ilizobeleya zaidi tu ni kusema. Sasa kama muntu wa akili anakufa, shi kunaisha. Anaenda na ile ma akili yake yote mu kaburi. Njo mana, bintu mingi bilikuya kurudia nyuma. Lakini Hampaté Mba alitutosha haya sana. Alikufa mu 1992 ao 1993. Ba nkambo yake ba mupokeye. Ali ba heshimiya sana na ma kazi ya kuba julisha ku batoto na ku ba nkana yabo.

Ukumbusho 8: ma mboka

Minawaza sasa asema kuko namna ya kuandika mambo yote ile inaikalaka mu bitabu ya bazungu ao ya bantu beushi benye kufanyaka buzungu mu kiswahili kietu kia mu njia. Ju ya ku avancer muzuri mu namna ya kuandika, ni ta anza sasa kuchakula tu mambo moja moja. Kwa mufano mi naweza kushimamia pa mambo ya ma samaki, ya ma mboka sa ma lengalenga, kibwabwa, tshitekuteku, mulenda, katete, nsombe, mudibudibu, matembele, matembele banki, mulenda ya karibu na midi, mulenda ya nchongo, mulenda ya ngaingai, nyanya, mushilu, ile mulenda inaikalaka yenyewe kufunga kofi. Lakini pa kuelezea muntu na ma mots vile ile ma mboka yote iko inashikirika mu kinywa iko nguvu sana. Utaelezeya muntu namna gani? Shi mpaka kama ye moya anaisha kupimako ao kama anaisha kula kintu kia ile namna oa kia kufanana nakio. Sasa ku ma ngambo ingine ya mukini yetu njo bantu bana kulaka ma nfumbwa na ma mboka ingine ile mishizobeleye mi luangu.

Ukumbusho 9: ma matunda na ma mboka.

Kama unaenda mu Matonge ya mu bulaya, ni kusema mule mu Bruxelles, utakutanisha biakula bia kwetu bia mingi sana. Bamingi bale beko banauzisha ile bintu biote, ni bantu ya kutoka ku ngambo ya Asie. Mina kumbuka muzuri asema, ile wakati nilikuwaka mutoto ku Lubumbashi, tulikuwaka na bantu mingi ya kutoka ku ile ngambo. Mu masomo yetu tulikuwaka na mutoto moya jina yake Keshav Narendra. Baba yake alikuwaka sa na kilema vile. Tena alikuwaka na ka appareil murishikiyo. Balikuwaka na magazin mule mu Lubumbashi. Mina waza asema balikuwaka beko bana uzisha bintu bimoya bia ma harufu ingine tu. Mama yake alikuwaka anavuala ma nkanjo mulefu sana. Tena ba nsula yake palikuwaka tu sa palikuwaka ka point kamoya hivi ka rouge. Yeye Keshav Narendrha alikuwaka wa ku Pakistan. Njo ile wakati nilijuwaka asema Capitale ya Pakistan ni Karachi. Lakini miaka inapita mingi sana. Mina shikiya asema kuko tena ba Indiens mingi sana mu Kinshasa na mu Lubumbashi. Tuseme tu asema ni bale bazungu ba ku chuyuka. Habana bazungu zaidi, tena habana bantu beushi. Kati yabo lakini kuna ikalaka bantu bengine beushi tu bakufuanana na shiye. Lakini mpaka ma nywele yabo njo iko ya teketeke sa ya bazungu. Turudiye mbele ku mambo ya ma bintu ya kuria bile beko bana uzisha mu Matonge. Uta kutanisha kule bilashi, mioko, nyanya, ngai nagai, nsombe, bitekuteku, igname, mankenena, dilombulombu, inswa, tunkubyu, minji, maembe, bitoyo, milonge, piripiri...Lakini bantu bana jiulizaka asema ile bintu biote bana bichungaka namna gani? Tunaisha kuona mu ma nsombe mayani ingine ile aina nsombe hapana. Banakuwa sasa beko tu na changa changa bintu ya kuachana mule ndani. Tena na fuashi inyewe ile beko na bi chunga ku mulango. Bengine asema, bana wekaka ma nsombe ile mu salle de bain tena mpaka mule mu baignoire mule. Njo pale miye shiuzake bintu ya mu Matonge hapana. Pa kuria nsombe ao mayani ingine, mpaka kama bana ni leteyabio kutoka directement kwetu. Ibi bia kuuzia mu njiya ao mu Matonge hautajua asema uko unakula nini. Lakini kua kusema peupe, mina penda sana ile chiakula ya kwetu. Hamuna ma dawa sa mu hiyi bintu tuko tuna kula huku ku Bulaya. Huku, hautajuwa asema uko unakula nini. Hata ma ndizi hiyi ya huku, mina onaka tu asema haina na butamu sa bua ile ma ndizi ya kukomeleya tu mupori ya kwetu.

Huku ku Bulaya kuko nako na ma restaurants ya bantu beushi. Bana pikaka ile bintu biote. Nilishikiya asema ku Bruxelles kuko restaurant moya bana pikaka bintu ya ba kasai: nsombe ya tshidibila, tshiomba tshia kabiola, ngozi ya mbuji, kichua ya mbuji, nkoni mutengela. Lakini kama unaendako, utakawa sana mbele ya bo kukupatia hata mayi hiyi ya kunwa. Mijiki lakini ni paka ile ya ba Tshiala Mwana, Kabasele Yampanya, Jibe Mpiana, Ngeleka Kandanda, Kabongo...

Ukumbusho 10:Ba nyama .

Tunapenda mbele kusungumuza mambo ya ba nyama. Ba frashi balikuwa ni ba nyama ya bazungu. Nfrashi eko beyi mingi sana. Tena pakumurisha, utafanya je? Na fashi ya kumuweka juu ya yeye kulala muzuri utaipata wapi? Bantu mingi banasemaka asema, frashi analalaka muenye kushimama. Hautaweza kumukutanisha eko mwenye kujinyolosha tshini hata mara moja. Ba frashi kumbe ni ba nyama ya bazungu ao ya mu ma cinema ya bazungu. Nyama muingine ilikuwa ni kalulu. Kama muntu eko na mashikiyo mulefu, balikuwa banasema kama yeye ni kalulu. Tena kama muntu eko na mbiyo sana, kama eko analukaluka ma ngambo ya kuachana. Ule muntu banaweza vile vile kumuita bu kalulu. Zaidi kama muntu eko anazala ku mwaka ku mwaka. Yeye vile vile bana muita asema ni kalulu. Kama muntu anaonekana kuwa mukalamushi sana, naye bata muita vile vile asema ni kalulu. Kalulu ni ma kabila yote inamukulaka. Mamba yeye ni mpaka balubakat njo balikuwa banamukuria. Njo utashikiya muntu anachambula mwenzake asema muria mamba we. Ngoji ya mamba balikuwa banafanya nayo bilato ao ma dawa ingine. Nyama yake njo bantu ya ku ngambo ya Malemba Nkulu, Manono, Kabalo....balipenda sana. Lakini mu ville ya Lubumbashi ilkuwa nguvu pakupata ile nyama. Imbua ilikuwa ni nyama bantu bengine ba ku kasai balikuwa kula. Shi bote hapana. Bantu ya mu ville, mpaka kama alikomeleya ku Kasai. Ilikuwa tena ni matushi ya kusema muntu asema kasai mulia imbwa we. Sasa bengine ba Kasai balikuwa bana jibu asema ata ku Japon na ku Chine banakulaka imbwa. Mpushi njoo bantu bote balikuwa bana ogopa. Zaidi kama anaanza kuliya bushiku, na kama eko na rangi mweushi. Ile macho yake ya kuangala mweushi ile, shi ni ya buloji tu. Sasa ukiende ku Gabon, utakutanisha kule bantu beko bana kula mpushi tu bien. Tena njo nyama ya kupokeleya nayo muntu munene sa ministre vile. Minashikiya asema ku Japon na ku Chine banakulaka mpushi tu bien. Kuko banyama bengine sa ba bandakwe, mpanya, makaka, zamba, mpombo-nfuko, kasha, ntembo, nsimba, nchui, mama na mbao, dizhuite, mbuji, nkondolo, ngulube, mpunda, ngombe, nyama ya pori...Bintu biko mingi mumukini. wakati ya kubitaya na kubiandika biote njo iko kiloko. Siku ingine, tuta rudiyaka pa hiyi mambo yote.

Umkumbusho 11 : Kanisa na Makanisa

Leo tuta anza masumgumuzo pa mambo ya ma kanisa. Jina kanisa inatokea wapi ? Ninawaza kama, ni jina inatoka ku jina ya misa. Ni bazungu, ba bwana mon Père (mumpele) balikuwa banasoma misa. Ile sala yabo, njo ilikuwa inaonekana asema iko na kilo mingi mu macho yabo. Pale muzungu wa kwanza alifanyaka misa ku Kananga ao Luluabourg, bantu balishangaka sana. Balionaka muntu wa ngozi ingine anashimama, kiisha anaikala, kiisha anashimama tena, tena anaikala. Kipande ana angalia yulu, kipande ana angalia chini. Kipande anakunjamisha mukongo. Mwisho yake anakuria ka mukate keupe, ana baima bengine. Kiisha ana kunwa tu mpombe mu ka nkopo ka kiuma, anabaima bale beko bana muangaliya. Bengine bantu ba kuuji balikuwa banasema asema, ule muzungu ali imba asema: na kuima divai, kusababu uko mtoto wa benyewe. Bantu balishangaka sana pa kuona muntu eko ana fanya mambo ya vile. Bote baliwazaka asema, ule muzungu eko anaomba ba nkambo yake.

Ile njo ile bantu balikuwa banaita asema ni misa. Sasa hiyi ma nkundi ingine ilizaliwa kiisha, njo ma kanisa. Ni kusema asema, jina ya ma kanisa iko tu sa ni matushi vile. Ni sa vile bantu banasemaka asema, ule muntu eko analala mu nyumba, lakini muingine analalaka mu kimbototo ao mu chiasasa vile ka Kasai banasemaka. Leo kuko ma kanisa mingi sana. Kuko ba shipiringa, ba témoins, ba society, ba neo, ba nzambi malamu, ba nzambi alleluia, ba kimbangu, ba malemba, ba du septième jour, bapostolo kundenga, ba wajehova, ba ngarenganze, ba pentecotistes, ...Tangu Mobutu ali ichika asema kukuye ma partis politiques mingi, na ma kanisa nayo ina ongezeka. Kuko sasa ile banaita asema ma églises de réveil. Bantu beko bana endamo juu ya kuisha mateso ile beko nayo. Beko bana ba elezeya asema, kama unapenda kupata bwana ao kuisha bu mashikini, ina pashwa kusali mingi na ku jêuner. Kama tuna angalia muzuri, ile ma kanisa inapita buingi bua ma misa ile ilitoka ku bazungu. Ni kusema asema, jina kanisa iko tusa ni matushi ya kusema kama ni ma nkundi ile aina inafuanya misa vile bazungu, ba bwana mon père balikuwa bana fanya. Tena ina onekana kuwa matushi ya kusema kama ile nkundi ni ya bantu beushi bo benyewe. Ni vile tu na shikiya mara moja moja bantu banasema kama, kuko kanisa na makanisa, ao asema kuko kanisa na tumakanisa. Ni namna moja bana sema kama kuko nyumba na bimbototo. Mu hiyi liste ya makanisa habatayemo ma musulmans. Zamani balikuwaka tu mpaka mu commune Albert ao mu kamalondo wa ntanshi. Bana ita ile commune asema ni kamalondo wa ntanshi, sababu ilikuwaka ni commune ya kwanza ya bantu beushi mu Elisabethville. Mambo ya ma communes na ya ma villes ya ku Katanga na ku Congo tuta isumbuliya siku ingine. Leo tuko tu mpaka na mambo ya makanisa. Nilianja kusema asema, zamani kulikuwaka ba musulmans kidogo sana. Balikuwa banabaita asema ni bauza. Ile jina ya bauza inatoka wapi? Bantu balikuwaka banasema asema, bo balikuwa bana uza bulongo. Ni bantu balitoikaka ku ngambo ya afrique de l'ouest. Njo kusema tu asema, ba maliens, ba shinangar (ba sénégalais), ba nigériens..tuseme tu bote bale baku ile ngambo ,balikuwa na jina moja tu : bauza. Kwa sababu balikuwa banasema luga banaitaka asema bausa. Njo vile ile jina ilianza kubalamata bote asema ni bauza. Sasa mu kiswahili kuuza shi ni kupeleka nfranga juu ya kupata kintu kile unatafuta. Tena bale bantu ya ile ngambo ya Afrika, bali kuwa banatafuta ma diamants. Kiisha bana uza ma mpango munene. Mule mu ma mpango, bali kuwa na tu ma milangomilango mingi juu ya ba bibi yabo. Ni bantu balipenda kuowa ba bibi sana na zaidi. Pawe kuona muntu eko na bibi moja tu, ilikuwa ni hasard. Ba mingi balikuwa mpaka na ba bibi mbili ao tatu. Bale bauza balikuwa banaenda mu ma sala yabo ku kazi tano. Pakuingiya mpaka unavula mbele bilato. Mishijuwe kama ni bia kweri ao kama ni bia bongo: bantu banasemaka asema ba musulmans abakunywake mpombe hata. Bana kunwaka mpaka mu bu fitsho. Siku moja nilikuwa ku Mbujimayi. Niliona muntu moja mwenye kuikala mu lupango yake eko anashikiya radio. Batoto ya muloko yangu bana ni elezeya asema, ule muntu ni muzulmani. Mina uliza asema: muna juwa je? Banasema asema, banaona vile eko na ka tache keushi pa nsula yake. Minauliza asema kale ka tache ni ka nchanjo banabachanjaka ao ni kintu kingine? Bananijibu asema, ni juu banatuangaka nsula pa bulongo wakati ya sala yabo ya mu kazi tano pale banakunjamishaka mukongo. Njo mana tunaona beko na ka tache ba nsula tu saa bantu bale balichanja vile balikuwaka bana bachanja ba mama yetu na ba baba yetu pazamani.

Kua kifupi tuseme nini pa mambo ya makanisa? Ile jina inaonekana kuwa tusa ni jina ya matushi ao ya kushukisha nayo ma kundi ingine kilo ku mbele ma kanisa ya bazungu. Zamani tumakanisa tulikuwaka ni tu bimbototo tu.

Ukumbusho 12: Bajamaa

Ile jina inatoka ni kua baba Placide Tempels. Miye nilikuwaka mutoto kidogo ile wakati ile nkundi ilikuwaka na kivukutu na moto mingi. Mara mingi, tulikuwaka tunaona vile bale bamama na ba baba balikuwaka bana enda ku masungumuzo yabo. Ile masungumuzo ilikuwaka inakawa saana. Sasa kama uko mutoto hautajua asema beko bana sumbulia mambo kani kule. Balikuwa banasema kama beko banasumbulia mambo ya bantu bakubwa. Sasa shiye na shiye tuna waza asema ni mpaka mambo ya ba bibi na bwana. Sababu kila mara kama unauliza mambo bana kujibu asema: ile mambo haikuangalie, ni mambo ya bantu bakubwa, una pashwa kujua asema ni mambo ya ba bibi na bwana. Juu ile mambo haba isemake mbele ya bantu bote sa vile bazungu banafanyaka. Ni mambo ya sekele. Sasa kulikuwaka mambo mingi sana balikuwaka banasema pa ba jamistes. Bengine asema balikuwaka beko na kabulana ba bibi na ba bwana. Njo pale ile mambo ili shimamiyaka zaidi. Biote bile hatujuwe kama ni bia kweri ao kama ni bia bongo. Kulikuyaka tena ma commentaires mingi bantu balikuyaka beko banafanya. Biote bile kama ni bia kweri, kama ni bia bongo, miye na weye hatujuwe.

Lakini tunajua asema bajamaa balikuwa na mafundisho mbalimbali. Ni mambo ya sikitiko pa kuona asema ile mafundisho ili patiya ma familles mingi nguvu ya kuikala pamoja itapoteya sasa. Sababu gani? Ni sababu bajamaa habazale tena batoto ni ki roho. Bana zala batoto ya ki muili. Ile ni kweli. Lakini hakuna tena ma jamaa ingine ile inaweza kuendelesha ile kazi na ile mafundisho. Ni kusema asema, bitabu biobinyewe habisemake ata. Inapashwa muntu wa kubisoma na ku bisemesha. Ile nkundi ili endaka weee na ku Kananga, ku Luiza, na ku Mbujimayi. Monsegner moja wa kule ku Kasai alikuwaka naye muntu wa jamaa. Baba Sommers, père moja muzungu, naye alikuyaka muntu wa jamaa. Père Gérard Meert wa ba Pére Blancs naye ni muntu alipendaka mafundisho ya jamaa. Abbé Paul Nkulu alikuwaka ku Grand Séminaire ya Lubumbashi naye alijuwaka mafundisho ya jamaa. Beko mingi sana, ba père bale baliingiyaka mu jamaa. Sasa kama baliingiyakamo je, njo pale batu balikuwa banajiuliza. Balikuwa banasema asema, pakuingiya mu jamaa, inapashwa kuya na mama ao na baba, ni kusema peupe asema inapashwa uko ni bwana ao bibi. Sasa bale ba père habana na ba bibi bali ingiyamo je? Mina waza kama kuko jibu moja tunaweza kuleta ku ile ulizo. Ni kusema kama, mafundisho ya jamaa ni mafundisho ya ki roho. Pale bantu ya jamaa bana sema kama jamaa ilianzaka kua Mungu, ni kusema kama aikuanzake mu Kolwezi ao mu Musonoie hapana. Ilianzaka mu mbingu. Mule mu mbingu hamuna mambo ya ba bibi na bwana hapana. Njo vile minaona nginsi tunaweza kujibu ku ile ulizo.

Baba Placide Tempels hakukuwa na bibi, lakini bantu yote ya jamaa balimu itshika kabisa. Kua kuona kwangu, ba baba mingi ba zamani balisikiaka mambo ya mungu muzuri pale balifuataka mambo ya mungu mu njiya ya ba nkambo. Ao tuseme asema, balifuataka ile mambo mu kintu kieushi, hapana tena mu kizungu hapana. Ni mambo ya sikitiko pa kuona asema mafundisho mingi ya jamaa, inapoteya. Kama una enda ku ma inchi ingine, utaona vile bantu bana eshimiya na kuchunga mambo ile balianza kufanya. Kwa mufano: nilisoma kitabu ya rafiki moja tulifundaka naye ku Tübingen mu Allemagne. Yeye anatokeya ku Irlande. Ana andika mambo mingi ya ba nkambo yake. Hata mambo ya ki pagano yeye ana i andika. Kua sababu, ni adisi ya ba nkambo yake. Hata kama kulikuwa ma nkosa, haina mambo, sababu hakuna muntu ule haikalake na nkosa mu bile eko anasema, ao mu bile eko anafanya. Sasa ba baba ya jamaa bote banaisha kufua ao bana zeka sana. Njo nkosa ile balifanya. Bana pita bila kuacha kizazi. Tuna juwa asema, nkosa hayina mpaka ku ngambo yabo. Kama habakubafanyake fujo mingi mu eklesia, kama bali endeleyaka na kuzalana. Lakini inapaswa kujiuliza kama ile kizazi ilitafuta kuya kia namuna kani. Njo pa mambo na pa mambo pale.

Ukumbusho 13: Maombi na sala

Iyi jina ya maombi iliingiya je mu misemeyo ya bantu ya Lubumbashi? Zamani, bantu bote balikuwaka bana sema kama bana enda kusala. Balikuwa bana sala shapele, ao balikuwa bana sala na sauti ya nguvu vile ba shipiringa ao ba nzambe malamu banafanyaka. Jina ya maombi ili ingiya zaidi ile wakati renouveau ina ingiya mu mukini. Wa kuanja ilikuwaka ni Abbé Mukulu Mwamba. Alisemaka yemoja asema, ni mama moja alikuwaka kumu elezeya kama yeye eko na kipaji fulani. Mu kusala kwake, asema ali anzaka kusikia ma sauti ya bafu. Njo pale ana anza kusema asema ina pashwa kila muntu anasala mu kiakuabo. Sababu gani? Ku hii ulizo yeye Mukulu Mwamba alisemaka, kama inapaswa kujuwa asema, ba nkambo beko banasema luga yabo mu kusumbuliya na Mungu. Sasa sa vile maisha yetu inatoka kwabo, ni bo njo banapashwa kupeleka maombi ya batoto yabo, na ya ba nkana yabo kua Mungu. Sasa kama unasala mu Francais, ile mambo yako yote ita baangalia mpaka ba Francais.

Ile shiku Mukulu Mwamba alitoshaka hiyi mambo yake, shiye bote tulishangaka. Hakuna muntu hata moja alimuitshikaka. Shiye bote tuli anzaka tu kutsheka. Ile saa ye luake alikuwaka tu mu ma sérieux ya kwerikweri, ma sérieux ya mbuji. Sababu mbuji hatshekake ye luake. Mambo yake yote ni paka sérieux. Ile mafundisho ya Mukulu Mwamba ye mwenyewe ali ipanga jina asema ni dynamique du ciel. Ni kusema : muikalio, ao zoezo ya mu mbingu. Ni ile wakati ma nkundi mingi ya sala ikaanza kuzaliwa mu Lubumbashi. Ku Likasi na ku Kolwezi kulikuwa ma nkunji kiloko.

Hamuone asema tuna weza kusema asema, ni ile wakati mambo ya jamaa ili anza kufua, njo ile wakati mambo mukubwa ya jamaa ikaendeleya mu jina ao mu formes ingine. Ni kusema nini ? Tuwaze mbele na kukumbuka vile mambo ya jamaa ili anzaka, na zaidi kujiuliza : na kintu gani kikubwa jamaa ilikuwa inatafuta ?. Nkundi ya jamaa ilianzaka mbele ya mugini kupata lipanda. Lakini mu mawazo ya nkundi mulikuwa zaidi ile niya ya kuwa na lipanda mu nginsi ya kufunda na kufundisha. Sasa ile ma nkundi ili anza kufua mu ma 1970. Ni mambo kani ilifuata kufika na mule mu ma 1970? Ile ma nkundi yote ilikuwa inatafuta lipanda mu ginsi ya ku funda na mu nginsi ya kufundisha. Ndio mana, tunaweza kusema asema ile ma nkundi yenywe kufuata mawazo ya dynamique du ciel, iko tu sa kizazi kia jamaa. Mina jua asema pa hiyi mambo panaweza kutoka bubishi bulefu sana. Lakini ni muzuri kubishanako ao kusema mawazo yako payari ya ku ichunga tu mu roho yako wewe mwenyewe.

Turudie ku mambo ya maombi. Ni ile wakati ma nkundi ilianza kuongezeka, njo ile wakati kulitoka na ma mots ao ma jina ya sasa. Tunaweza kusema kua kifupi asema, kama kunatoka nkundi ao mafundisho ya sasa, kutatoka vile vile ma jina ao vocabulaire ya sasa, ju ya kutaja ile mambo ya sasa na tena ju ya kuonesha asema ina achana na ile ya zamani. Ni vile bantu bakaanza kusema asema bana enda ku maombi. Sababu gani? Ni kwa sababu balijua sasa ginsi ya kusungumuza na Mungu. Ni kwa sababu balijua sasa ginsi ya kutengeneza kifulushi ya masala ya kutuma ku mbingu. Ile kifulushi ya ma sala ilikuwa ina pitshiya mu mikono ya ba nkambo. Njo mana balipenda ikuwe ma sala yenye kufanywa mu ma luga ya ba nkambo. Sasa vile bantu balikuwa banawaza asema sasa banajua namna ya ku sungumuza na Mungu, na tena kama mungu atabashikiya, bantu mingi bakaanza kusema zaidi asema banaenda mu maombi. Banajuwa sasa asema kuko ule beko banaomba na ata bashikiya.

Mina jua asema kama muntu anasoma hiyi mistari anaweza naye ku nijibu asema ile mambo hayina vile hapana. Hanaweza kusema kua mufano asema, mu ile ma nkundi bantu bote haba sale mu kia kuabo. Tena kuko bamingi beko banasala mu Francais. Na ma mimbo ingine ni ya mu Francais. Pakuona biote ibi, tuna weza kusema asema mambo ya kulanda ao ku distraire bantu asema jina maombi ni jina iliingiya mu misemeo ya bantu mu ile nginsi tulipima kumishikirisha haina vile hata. Sasa uni elezeye, kua kuenda ni wapi? Mambo ya kweri iko ngambo kani? Kama muntu anasema asema mu ma nkundi ingine bantu balikuwa bana imba na ku sala mu Francais, ni kweri. Yote ile ni kwa sababu kulikuwa nkundi ingine ao mouvement ingine mpaka mule mu Lubumbashi. Ile mouvement ilikuwa charismatique ya kutoka ku bulaya. Sasa ma bitabu, na ma mimbo yote bilikuwa tu ni mu ile luga ya bazungu. Sasa inakuwa wazi asema mambo iliweza kuchangana. Mu Lubumbashi mule shi mulikuwa ni mu changachanga. Ma kabila, ma coutumes, ma bikario, mawazo, ma kanisa , mazowezo...biote bili changanachangana mule. Njo kusema hayina tena mambo ya ku changaa pale bantu beko banaimba ao kutuma maombi mu ma luga mbalimbali.

Lakini tukiangalia ma nkundi sa ile ya baba Amisi wa mu Kamalondo, ile ya Mukulu Mwamba wa mu Bel Air, ao tena ile ya Mukulu Kasongo wa mu Gécamines, kule hakukuye mambo ya kuchangachanga. Tubakiye mbele pa mambo ya Kasongo. Kule kuli toka namna ingine ya kusema na kuimba. Ile namna ya kusema ni kuimba ili onyesha kama kulikuwa namna ingine ya kuishi, ya kuwaza na namna ya kuona maisha. Kua Kasongo balikuwa banasema zaidi swahili bora. Lakini hayikukuwa bora zaidi. Mukulu Mwamba na Alimasi bali tokeyaka ngambo ya Kongolo na Kalemie. Kasongo yeye alianzaka kusoma bible kila shiku. Sasa ile bible ni yenye kuanjika mu kiswahili ya kongolo na kalemie. Tena baba yake na Mukulu Kasongo alikuwaka mu jamaa. Mafundisho ya mu jamaa, ili kuwa yote mpaka mu kiswahili. Njo maana yeye nayeye alibeba ile héritage, ile mambo yote alikuwaka anashikiya kubutoto buake. Ile kiswahili ya mua Kasongo bantu bote baliweza kukishikiya tu bien. Kili kuwa kina onyesha kama bale balikuwa banaenda kufwata mafundisho yake, balikuwa na namna yabo ya kuona mambo ya mu vie.

Tubebe mbele tumifano tuloko tua luga ile bantu balikuwa banasema kule kua Mukulu Kasongo. Ile fashi bantu balikuwa banasala mara moja moja ao banatuma maombi yabo, bali kuwa bana iita asema ni mu jangwa. Sababu gani? Kasongo alianzaka mbele kusali mu misa ya Notre Dame de la Paix mu Gécamines. Sa vile ali onekanaka asema eko na kichua nguvu, habakupatanake na Askofu Monsegner Kabanga. Njo pale bali mufukushaka mu ile misa. Njo pale yeye naye aka anzaka ku sala na nkundi yake inje. Sasa pale inje balikuwa bana paita asema ni mu kiwanza. Mu mashiku ile balikuwaka beko bana pitshisha siku mujima pasipo kula kintu ao kunywa, njoo ile mashiku balikuwaka bana enda ku ngambo ya tuburi, mu pori. Ile pori, mule hamukukuyake kintu hata kimoja, balikuwa bana iita asema ni jangua. Kuli tokaka na ka muimbo kamoya asema: Mu jangwa muko na nani? Mu jangwa muko Bwana.

Mina ona asema, inapashwa kuachiya hiyi mambo mbele hapa. Tuta endeleshakayo mara ingine. Sababu kuko mambo mingi sana. Lakini mina tafuta, mbele ya kuachana, kukumbusha tu bupeshi bupeshi asema,ile namna Mukulu Kasongo ali anza kufundisha ni mu style ya ba jamaa. Sababu kulikuwa kila mara ma thèmes ya mafundisho juu ya kukomesha bantu mu imani yabo.

Ukumbusho 14: Kulakuisha na kuditunzisha kwa nganga

Mina kumbuka mambo moya ilifikaka mu 1976. Ni zamani lakini. Shibote tuko tunaenda na kuzeka. Hakuna mwenyewe eko anabakiya kiyana hata moja. Ili kuwaka mbele ya ma examens d'état. Des moja hivi (DES njo kusema ni kufupisha jina ya ba dada, ba soeurs yetu bale tunaita asema Desoeur. Inapashua kusema tu asema DESS. Ile S yakumuisho inapasuwa kuzikilika sa vile ba Kasai bana semaka kua mufano asema 'wewa's'). Turudiye ku mambo ya ule Dess wetu. Ilikuwaka mbele ya ma examens d'état ile batoto ya leo beko banaita kua kufupisha asema ni exetat. Ule dada anaingiya mu salle d'études ya ku masomo kule alikuyaka eko nafunda. Hanakutanisha banaisha kumuiba sakoshi yake na ma cahiers na bitabu biote. Sasa uta fanya nini ile wakati? Examens d'état nayo inaisha kuanza kununka tu peupe. Benjake bote ba mu masomo balikuwa besoin na ma kaye yabo juu ya kufunda. Ile wakati nayo, hakuna hata muntu moya hali wazaka ku musaidiya juu ya yeye kuenda kufanya hata ma photocopie mu Gécamines ao mu KDL. Ile mawazo yote ilikuwaka mbali sana na zaidi. Njo rafiki yake na ule DES anamusaidiya mbele kwanza ku copier ile ma cours yote balikuwaka banaisha kufunda. Ule rafiki yake alikuwaka luake angali mu cinquième. Sasa huyu muinyewe mwenye mambo ali pashwa kufanya je? Kuacha ile mambo ipite tu hivi? Hapana, ndugu yangu. Mu dunia hamuikalake vile hapana. Bule ni bu pumbafu. Inapaswa kujua asema, kuko mambo mingi sana ile iko inafanyika. Hauta jua asema mwenyewe eko ana ku kombanisha pale ni nani. Vile ile mambo ilifanyikaka majuma kiloko tu mbele ya ma examens d'états, saa ingine bali wezaka kuya na kumu iba hakili yote siku ile ya examens. Njo pale ule DES akasemake asema, inapashua tu kuenda kulakuisha. Juu kama uko na mambo ya vile, una enda ku ba Pères, habana na kile batakuelezeya kia kabaila. Bata kuelezeya tu asema usali shapele ao ubarumiye. Lakini kama unapenda kujuwa mwenewe ali fanya ile kitendo, ina pashua tu kuenda ku lakuisha kua mufumu.

Njo pale ule dada aliendaka kuuliza mu Kamalondo wa ntanshi kule banalakuishaka. Bakaenda kule na mukubwa yake. Ule mukubwa yake naye alishikiya ka boka sana. Aliwazaka asema, kama anakatala asema niko mu kristu, kiisha ule muloko yake anashinda examens, itakuya tu mambo ingine. Itakuya asema kama aliendaka tu kulakuisha, kama haba kupate ile mambo yote. Sasa mukuenda kulakuisha namo, shi ni mambo ingine nayo ile. Hautajuwa kama ma bintu ingine haitakulamata. Sa ingine ma ndoto ya ma modèles ingine ita anza kukufuatafuata bushiku. Pale balifika kule kua ule mufumu, ule mufumu ali baelezeyaka asema, anajuwa kinyewe kile banafuata. Haka bapatshiya kibuyi kimoya hivi muko mayi. Kiisha akasema: muangariye mpaka humu mu kibuyi. Mushi angalie ku mpembeni hapana. Kama bali muonaka ule mwivi ao kama haba kumuonake, miye na weye hatujuwe. Lakini mufumu alilakaka asema bata mupata ule muntu. Na leo huyu mishaya shikiya asema ule mwuivi alionekanaka. Lakini bali lipaka nfranga mingi. Tena ule DES aliwezaka ku examens d'état yake tu muzuri.

Sasa tujiulize mbele: iyi mambo ya ku lakuisha ni ya kweri ao ni ya bongo ? Bengine asema bana onaka bantu, zaidi banamuke bazee, beko bana enda bushiku mu mpepo tu. Tena asema bana fanyaka ma voyages yabo beko pa bifuakiyo. Bengine nabo asema kulakuisha ni kujua muzuri bile bintu bina ikalaka biko binauji bantu. Njo mana ba mufumu banaikalaka beko na shikiya mbele muntu mashiku mingi. Rafiki yangu moya ali anzaka kushindwa masomo sana. Siku moja, anaenda kuonana na Askofu moja. Ule naye ana muelezeya asema, ende mbele ku mukini yabo juu ya kusumbuliya na ba ndugu yake. Bengine na bo asema kulakuisha ni mbele kujuwa madawa ya miti yote, juu ya kutunza bantu. Sasa ule ni mufumu ao ni nganga? Na ba nganga nabo banasemaka asema, pa kujua ma dawa inapashwa mbele unalala muzuri, unaomba, njoo batakuonyesha mu ndoto miti ile unapashwa kukata juu ya kutunza nayo bantu. Bote mbiri beko na tumika na ma nguvu ya kutoka ngambo ingine.

Ukumbusho 15: Buloji bua beushi na bua bazungu

Mara mingi, kama muntu anaenda kua mufumu, bata muelezeya jina ya muizi wa bintu yake, ao jina ya muloji. Muloji ni nani? Hiyi jina iko mu ma luga mingi sana. Muloji ao ndozi ao ndoki...ni ule muntu eko na ma nguvu ao ma puissances ya namna ingine. Zaidi ni ule muntu eko anatafutiya bantu bengine bibaya. Ni ule muntu eko na kiricho. Muntu ule eko na landiyanaka mambo. Tuseme tu kua kifupi: ni ule muntu eko na roho mubaya. Ku Kamerun banasemaka asema: kuko bantu bana ikalaka na nguvu ya kuiba nguvu ya bantu bengine. Munaweza kuya muko munatumika mu mashamba, unaona mwenjako anarima mituta mingi sana tena bupeshi kukupita weye. Sasa ule menjako, kama eko mukonde sa nsosomani, weye uko maftumbo sa ngulube, uta ba onyesha bantu asema ile mambo ao ile nguvu ya kurima iko ya namna gani? Ao utasema asema ile nguvu inatokeya wapi? Njo vile na ku mambo ya masomo. Zamani, ilikuwaka tu kama muntu eko na akiri sana, balikuwaka banasema mara mingi asema ule muntu ni muloji. Utashikiya tu bantu asema kubafulani banafanyaka madawa sana. Njo pale unaona bote beko banaweza masomo, tena beko banayisha bupeshi bupeshi. Ao kama muntu eko najuwa mambo ya bengine bupeshi. Hauja muelezeya mambo yote peupe, yeye anakufasilia vile ile hadisi inapashwa kuendeleya. Muntu wa vile naye balikuwa bana mutaja mukusungumuza mara moja moja asema ni muloji.

Hiyi ma mifano tunatoka mukuleta hapa ina onyesha wazi wazi kama ule muntu bana taya asema ni muloji, ni muntu eko mwenye kuwa na nguvu ao na akili yenye kupita bile bantu bengine banaweza kushikiya. Na zaidi kama anabeba ile nguvu yake ana anza kutumika nayo juu ya kuteswa nayo bantu bengine. Kuko mambo moya ilipitaka mu 1992 ku Kinshasa. Ilikuwaka ni mambo ya kushangaa, tena mambo ya ncheko tu. Mushikiye tu vile bantu bakubwa bali anza ku angayika na roho, juu tu ya kuchunga cheo. Mobutu ali onaka asema bantu haba mupende tena hapana. Sasa kulipashwaka kuya ma votes ya ku conférence nationale. Muntu moya anakuya kumu landa Mobutu asema, kuko muntu moya eko na dawa, eko na bijimba ile anaweza kumufwanishiya vile bana fwanishiyaka bale beko na cheza futubolo juu ya bo kuwina. Ule muntu alikuwaka ku Mwene Ditu. Njo vile baliendaka kumutafuta ule muntu. Jina yake ilikuwaka ni Kanku nawaza. Mara ingine, mina kotola. Benyewe balikuwaka kule asema, ule Kanku alifanyaka mastajabu mbele ya Mobutu. Asema balifanyaka ma votes mule munyumba ya Mobutu. Ule Kanku anachanger mapapier yote pale palikuwaka majina ingine. Mapapier ya votes yote inakuwa mpaka na jina ya Mobutu. Njo vile bantu bote balikuwaka banasema. Lakini ule Kanku ali ombaka asema, balete mbuji mweupe washipo tache hata moja, juu ya mambo munene inyewe ya ma votes ya ku conférence nationale. Bakatafuta mukini mujima weeee, bakapata mbuji ku Kalemie. Mobutu hakatuma avion mujima juu ya kwenda kumutafuta ule mbuji. Sasa ile wakati banafika ku aéroport ya Njili ku Kinshasa, banashuka tu hivi, ule mbuji ana fanya nini, anaanguka. Anakufua pale pa kiwanja. Bote banashutuka. Bale bantu balitumaka kwenda kumubeba ule mbuji mweupe pasipo tache, banaanza kukimbiya kimbiya pale. Banakatuka mbiyo yashipo yashipo kuangariya tena kumukongo.

Kuko tena mufano ingine. Bantu balikuwaka banasema asema, kama muko na match ya futubolo, inapashwa kwenda kulala mu local. Ile wakati muko mu local, munaweza kwenda kua mufumu, ao kwa nganga ao kwa muloji juu ya yeye kumifwanishiya dawa ao bijimba. Mara mingi, bantu balikuwaka banasema asema, mukienda kule, bata mi onyesha kibakuri kimoya hivi mule muko mayi yenye kuchanga na ma dawa ingine ile haujue. Sasa muta anza kuona match mujima vile itakuwa. Kama unabeba nshindano unaweza kumutuanga ule joueur unapenda kuregeza. Lakini kulikuwaka tena na ma bijila bia mingi. Kua mufano balikuwaka banasema asema, inakatazwa kusumbuliya na banamuke ao tu kubachekesha. Hata unaona ule mwanamuke una fahamu, ni kupita tu mu sérieux ya mbuzi tu. Kama una haribisha bijila ao kijila kimoya, mambo yote ina haribika. Biote bita kuangukiya mpaka weye. Ile mambo ilikuwaka sa ile ya pa kuenda kuchuma bisongole. Mu Ruashi bali anzaka kutu elezeya asema, kama una ona kisongole kia ku ivia, hapana kuanza kucheka. Inapashwa kufurahiya tu mu roho. Hapana kuanza ku criercrier asema, kiokile mina kiona. Kama una anza mambo ya vile, uta shangaa tu pale utafika karibu na mutshi ya kisongole. Utakutanisha kisongole au kibichi ndani, ao kina isha kuoza. Nkosa ni ya nani? Nkosa ni yako, juu haukufuate vile balisema. Ku Kasai banasemaka asema : uya muyaya nganga, kuvu kupa nganga cilema. Ni kusema : utembeye mpaka vile nganga alikuelezeya, juu ya ushikuye kumupatia yeye nganga nkosa.

Kua kifupi, tuseme asema muloji ni muntu ule anaonekana kuwa na nguvu ao akili ao baati ile bantu bamingi habana nayo. Njo maana bantu balikuwa banasema asema, kuko na buloji bua bazungu. Ile buloji ya bazungu ni ya ma miotoka, ma appareil yabo, ma avions..ma bintu moya hivi haushikiya asema bina toka wapi. Bazungu ni benye kubapita bantu beushi ku mambo ya vile. Shi ni baloji nabo.

Sababu gani banasemaka asema, inapashwa kutosha buloji? Kutosha buloji mana yake ni kutapikisha muntu bubaya bule eko nabo ndani yake. Leo huyu tuko tuna shangaa pa kuona ma églises de réveil iko mpaka inafuata batoto na kubasema asema, beko na buloji. Maana yake: beko na ma nguvu moya hivi ile bantu habawezi kushikiya?. Kama kuna toka baati mubaya mu famille, mara ingine bata tafuta muntu wa kuangushiya ile mambo. Ni ule bana tayaka mu Francais asema bouc émissaire. Sasa muntu wa vile inapashwa atoshe bubaya bule eko nabo ndani yake. Kuna ikalaka ma mambo ya ku landiyana na ma mambo mingi mingi tu. Utashikiya asema, inapashwa muntu fulani atapike buloji. Kumbe pale ye luake hana na mambo. Mambo yenyewe iko inaleta sikitiko ni zaidi ile mambo ya batoto beko bana kimbiya ku ma nyumba kule beko banabasema asema beko na buloji. Yote hiyi ina onyesha asema tu nafika mbali sana. Tuna acha mambo ya ki asili ile ilikuwa muzuri. Tuta rudiya pa hiyi mambo na masumgumuzo ya kia kwetu mara ingine emu juu ya kujikumbusha.

Tueleze mfano ya muinsho mu hiyi mambo ya bulozi, na mambo ya ba nkambo. Mina jua asema mama moja alikatalaka ile mambo ya kumulandiyaka na buloji. Kulitokaka tu mambo mu famille asema, bwana hana tena muzuri, kumbe ni ule bibi beko naye njo anajuwa kwenyewe kule ile baati mubaya inatokeya. Bana ita Pasteur moya hivi wa église de réveil juu ya kukata ile mambo.Ule pasteur anaombeya bwana mule mu nyumba. Anaomba, anaomba, anaomba, anaomba. Anakawa saana. Kiisha anasema asema, bwana luake hana na mambo. Kiisha anachofweya kule kuko bibi juu ya kumuombeya naye. Kunapita tu ka kipande kafupi, anasema asema, ule bibi eko tu na mambo. Pale pale ule bibi anamulukiya pasteur mu nshingo. Ana muvinya kakono. Anasema asema, ile ni injustice sasa. Pakumuombeya bwana, anakawa saana. Sasa pabibi, njo anasala tu cinq minutes tu. Alla? Ile shi ni kumubenga pa bantu. Ile sala ika isha pale pale. Munaona kule tuna fikiya sasa na ile mambo ya kwanza kutayana ma buloji.

Tuendeleye mbele tena kiloko. Kutosha buloji inaweza tena kusema asema, muntu anakunwa mbele ye moya tu mpombe ao anakula ye mwuinyewe mbele ka kipande ya nyama ao ya bukari mbele ya bantu bengine ba anze nabo. Maana yake, kama mu ile chakula muko kibaya kitamukamata yeye moya. Ni mu ile namna bana semaka asema, inapashwa mwenyewe ule anapatia bantu chakula ao ule ali baita kwake, atoshe mbele buloji, atoshe mbele bubaya bule bunaweza kuya mule ndani.

Ukumbusho 16: Mambo ya ba nkambo na mambo ya bazungu

Leo tutapima mbele kukumbuka mambo ile banaitaka asema, ni mambo ya ba nkambo. Mina jua asema ile mambo ya ba nkambo bana iitaka tena asema ni mambo ya ki asili ao mambo ya kia kwetu. Mambo ya ba nkambo ni kusema, kama ile mambo ina achana na mambo ya bazungu ao mambo ya mu kizungu. Mambo ya ba nkambo ni ile mambo yote balikuwaka banafanya mbele ya bazungu kuingiya mu mukini. Tulete mifano kidogo juu ya hiyi maneno tunasema hapa ishibakiye tu mu mpepo bule.

Mu mwaka 1986 kulikuwaka feti ya jubilé ya diocèse ya Lubumbashi. Tuli muitaka baba mufwankolo mwana wa lesa, juu yayeye kucheza théâtre pamoja na bale bantu ya nkundi yake. Majina yabo inyewe mina anza na kuisabu. Kulikuwaka ba Kalwasha, Bibi Kawa...Mishijuwe tena asema bale bengine ni ba nani tena. Miaka njo inapita bwuingi sasa tangu ile mambo yote ilifanyika. Ile théâtre bali iita asema, ni Eglise et développment. Sasa tuliwaziyaka asema, bata tuonyesha namna ile ekleziya ao kanisa ina saidiya bantu kusudi baende ku mbele. Lakini balichangachanga mawazo mingi mu ile théâtre yabo. Mambo ilikuwa pale tu ku mwanzo ya ile muchezo ilikuwa juu ya kuonyesha asema, mbele ya bazungu kuingiya mu mukini, bantu beushi balikuwaka na namna yabo ya kuishi. Njo mana kumwanzo ya ile théâtre mufwankolo mwuinyewe anaonesha vile balikuwaka bana omba mungu. Mbele ya kwenda ku lumbata ba nyama mu pori, bantu ya zamani bali kuwaka bana omba ba mijimu ao ba nkambo babaonyeshe ma njia ya ba nyama. Ile kintu baba mufwankolo ali onyeshaka, sababu hakupende baseme kama bu muntu buli anza tu ni pale bazungu balifika ku mikini ya bantu beushi.

Mpaka ile mawazo yake ni mawazo tena muntu moya wa ku Nigeria aliandika mu ma bitabu mingi. Jina ya ule muntu ni Chinua Achebe. Huyu baba alipata prix moya munene ya bale bana uzishaka bitabu mu Allemagne. Minakumbuka vile alikuyaka kubeba ile prix yake kunapita miaka mbili ao tatu. Kitabu yake ya kwanza kina eleza hadisi ya Okonkwo. Ule Okonkwo kabila yake ni Igbo. Ule Okonkwo ali zobeleyaka mambo ya ba nkambo yake. Kulikuwaka mambo ya kulakuisha. Kulikuwaka mambo ya kuowa ba bibi mbili ao tatu. Kulikuwaka mambo ya ma bukonvi na bantu ya ma kabila ingine. Chinua Achebe anaonyesha mu kitabu yake vile bantu balikuwaka banakata mambo yenye kuangalia mugini yote mu kiwanja munene mule bantu bote beko nashikiya maneno ile beko bana eleza. Tena muko mambo ya ncheko mu ile kitabu. Pa fwashi moya hivi, ana onyesha vile bantu balipendaka kula mingi sana. Sasa anasema, kama ile wakati balikuwa bana onana mu nsoko, kila muntu alileta bintu sa ma bukari vile. Lakini ile ma bukari ilikuwa mingi sana. Kama una buweka mu nsani yako, hauta ona ule muntu eko mbele yako ao ule eko ngambo ingine. Sasa ile mambo yote, ile mazowezi yote inakuya ku changer ile wakati bazungu bana ingia mumugini. Ndiyo maana tunaweza kusema asema, ile kitabu yake mu kiswahili ni "Bintu bina pomoka". Mu ki angele ni "Things fall apart". Kama unasoma muzuri ile kitabu, utaona asema kila kipande, kila chapitre yakio ina eleza na kushikirizisha tabia moya ao mbili ya ba nkambo yake. Ye mwenyewe ali semaka asema, alitafuta miaka mingi juu ya kuona bale bantu bapuji, bale basenji, bale bantu bashipo akili, bale bantu beko tu sa nyama, bale muntu moya wa ku pologne, jina yake josef conrad alitayaka mu kitabu yake. Mu ile kitabu anasema tu peupe asema kule ku Kongo ni mu katshi ya ngiza tu. Kama ni yeye mwuinyewe alipenda kuleta mwangaza mu ile ngiza, miye naweye, hatujuwe. Sasa baba Chinua Achebe alisema asema, hakuone ile ngiza hata. Aliona tu mu mambo ya ba nkambo yake ma tabia muzuri na ma tabia mubaya. Ni vile tu ku ma mikini yote. Hakuna bale beko tu na bizuri pa bio. Hakuna bale na bo beko tu mpaka na bibaya pabio. Biote biko bienywe kuchangachanga sa mu ballot ya nkombo vile.

Tuendeleshe kidogo mbele hiyi mambo ya baba Chinua Achebe. Mu ile kitabu yake ya "Bintu bina pomoka", anaonesha tena vile ma tabia ingine ilikuwa kuingiya mu mukini. Ule Okonkwo alishinda namna ya kuichika ile mambo ya sasa. Kulikuwa kanisa ya sasa. Batoto bana anza kwenda ku masomo ya bazungu. Habapende tena kufanya ma bukonvi juu ya kuwina bantu ya ma mikini ingine. Biote bile, bilimupita Okonkwo kichua. Siku moya ali uwaka muntu. Njo bantu bana fuata mbele ma tabia ya ba nkambo. Bakamutuma ku mugini ya ba muyomba yake. Okonkwo ali enda kukawa kule miaka saba mujima. Nikipenda kuendelesha hiyi hadishi ya Okonkwo, hatutaisha hiyi mambo leo hapana. Kumbe tuachiye mbele hapa. Kikubwa nilipenda kusema, ni kama hakuna kabila hata moja ile haina na mambo ya ba nkambo. Angalia ile wakati baba Placide Tempels alianza kufundisha mu namna ya ki jamaa. Bale bali mushikiya balisema bote na furaha kama yeye anafundisha ao anasema vile ba nkambo balikuwa banasema ao kufundisha.

Mu mambo ya ba nkambo muko bizuri na bibaya. Ni changachanga to sa ballot ya nkombo. Mu namuna ya kueshimiya bantu bakubwa mina ona kama ni muzuri kabisa. Lakini inapashwa mukubwa naye aji eshimiye kama anapenda bamueshimiye. Njo pale bantu banasemaka hata leo mara moja moja asema, inapashwa muntu aji eshimiye mbele ye moja. Ao kama mama wa batoto ana anza kutafuta kurudiya ku bu kiyana na kusabu asema miaka yake ya kufanya michezo ao miza ingine pa bantu inaisha kupita. Ule mama wa vile bata muelezeya hata mu kibengo asema inapashwa aji eshimiye mbele. Hata kama baba ana anza naye kujiwaziya asema maisha njo ina anza sasa, kama bana anza kumukutanisha mu mafashi mule batoto ba ma série 7 ao série 8 beko banapenda mbele kufurahisha mwili na maja, ule baba bataweza kumusema mbele naye mu kibengo asema inapashwa anze mbele kujieshimiya.

Tubebe mufano ingine ya mambo ya ba nkambo. Pakuenda kuowa habendake we moya hapana. Inapashwa una enda na bazazi ao na bantu ya famille yako juu ya kupeleka mari. Ku buko habendaka weye moya hapana. Kule, bata mipikiya nkuku. Tena inapashwa kumukula tu yote. Kama hamuna ba nguluma, kama muna shindwa, batamipatshia ile ma nyama yote inabakia juu ya mweye kwenda nayo. Mu nkunku mwuinyewe mule muko ka kipande kamoya kana pashwa kuya mule mu kiungu. Mishijuwe vile banakaitaka mu kiswahili. Mu Ciluba ni ka dinkula. Mu ki francais ni ka foie. Ile ndowa ya kufwantana na mambo ya ba nkambo, ndowa ya kupeleka na mari, mina ona iko muzuri kupita iyi ya mu kizungu. Tuna anza tu kushutuka asema kijana fulani na chéri wake wa paile nyumba panaikalaka mutshi, banaisha kuowana. Ao tena munamuna ya kuzika bantu. Ma biriyo ya kufuatana na mambo ya ba nkambo, iko inapatia muntu nguvu. Bantu beko banakuya kukularishako mbele mule mu kirio. Hautaona asema uko weye mwenyewe hapana. Lakini hatuwezi kufitshika asema kunatokaka mafujo mara moja moja. Zaidi kama kulikuwa batoto ya ba bibi ya kuachana.

Kua kifupi tuseme aseme, mambo ya ba nkambo ni ma nginsi balikuwa bana ikala, tena na ma ginsi balikuwa bana kata ma mambo ya kuachana: namna ya kwenda ku lumbata ba nyama, namna ya kwenda kuowa ao kwenda ku bukweri, namna ya kuzika bantu, namna ya kuisha ma bubushi mu famille, namna ya kurudisha masikilizano kati ya bibi na bwana, ao kati ya bazazi na batoto.

Ukumbusho 17: Mambo ya Mungu na mambo ya shetani

Sasa tuna penda mbele kuendeleya na hiyi mawazo ya kujua asema, mambo ya ba nkambo ni mambo gani? Ile mambo ya ba nkambo bana i ita mara moja moja asema ni mambo ya shetani. Mbele ya kusema mambo yote yote, tunapashwa kujua asema jina shetani ni jina yenye kutoka ku ba arabu na ku bajuda. Hata jina la malaika nayo ni yenye kutokea ku ile ngambo. Mu kila kabila ya ki Afrika kulikuwa ma jina ya kutaja nayo Mungu ao bile biumbe biko naye karibu. Ni kusema asema, mu ma luga sawa ciluba mulikuwa tu ni Mungu na mizimu ya ba nkambo ao ba nkambo. Pa hiyi fuashi mina ogopa kiloko kutaja jina la mizimu sababu kila mara muntu anataja ile jina ina lamusha mawazo ya biumbe ya roho mubaya. Kumbe tuache mbele hiyi bubishi. Tuta buendeleshaka siku ingine. Bia kusema, na bia kubishana biko mingi sana. Sasa mu iyi ma religion ya kutoka mbali, banasema kama kuna ngambo moya ba malaika na ku ngambo ingine shetani ao bale banamutumikiya. Pa ihi mambo tuta kawiyaka po siku ingine. Tuna jua asema, mu ma luga ingine kanisa ya ki katolika ili ingiza ma jina ingine. Kua mufano kule ku Kasai banaita ba père asema ni ba nsaserdose. Habakupate jina ingine sawa ku Kinshasa kule bana baita asema ni ba nsango ao ba nganga nzambi. Sasa ku ngambo ya ba ma soeurs, beko na ma jina mbili kule ku Kasai. Bana baita asema ni ba masele ao badiambika. Badiambika mana yake nini? Ni kusema bale bantu banajibebeya miziko bo benyewe. Bale banajituika bobenyewe. Njo kusema, hawuweji kuya kulandiya muntu muingine hapana. Mushikiye mufano ingine: Ku Lubumbashi bantu ba nasema asema, muntu anafanya zambi. Kufanya zambi ni ku kosa mu ginsi unatendea bantu bengine ao mu ginsi una jitendea wewe muinenyewe. Lakini kule ku Kasai beko banaita zambi asema ni mpekato. Ni jina inatoka ku bazungu ba latin. Na vile vile bana sema banjelo juu ya bamalaika. Na banasema bansantu juu ya batakatifu. Ku ngambo ingine ya Kongo kuna mukini moja ili pata ma jina mbili. Ni ngambo ya ku Bas Congo. Kuna ngambo moya ya mayi munene ya fleuve Kongo banaita Inkisi, na ngambo ingine ni Kisantu. Ni ba pères jésuites baliletaka ile majina. Ku ngambo moya, njo kule balibapokeleyaka muzuri. Bantu ba ile ngambo ya mutoni njo batakatifu tuseme tu. Ndiyo maana mukini inabeba jina ya Kisantu. Vile kila muntu anaweza kuona kama, hiyi jina haina ya kutoka ku bantu beushi hapana. Ni jina ya kutoka ku bazungu ba ki latin. Alafu ile jina ingine ya Inkisi ina toka ku bantu bobenyewe. Ni kusema asema, mu ma luga ya barabu, bayuda, bazungu balatin, kuko saa nvita vile katika biumbe bile biko karibu na Mungu. Kuna ma partis politiques mbili, ya muzuri na ya mubaya. Ndio maana banasema mara mingi asema kuko mambo ya Mungu na mambo ya shetani.

Sasa tufuate mbele muzuri hiyi mawazo juu ya kuona kama tunaweza kuitshika ao hapana. Hatutaweza kusumbuliya mushiku moya mambo yote hiyi hapana. Lakini tunapima tu kuleta mifano kidogo kidogo. Mishijue kama munaisha kushikiya jina ya muntu moya jina lake Mabika Kalanda. Hapa tuko tunasema hapa, anaisha kufua. Ali anjikaka kitabu kimoja jina lakio mu francais "la remise en question", ni kusema tushi itshike bintu pasipo kuulizisha. La remise en question maana yake ni "Kuulizisha. Mpaka ye muntu moya ule, ali tosha tena kitabu kimoja jina yakio mu francais ni " La révélation du tshiakani ". Mu ile kitabu, anafuata zaidi mambo bazungu bawili baliandikaka pa mawazo ya bantu beushi. Bale bazungu jina labo ni Fourche na Morligem. Lakini kule kwetu bali pataka majina ya bantu beushi kwa sababu bantu bali baitshikaka. Ni vile inafanika mu ma kabila mingi. Kama uko muntu wa inje ku famille moya, lakini bantu ya ile famille bana ku itshika bote na roho moja, batakuingisha mule mu famille. Uta zalikwamo. Batakupanga jina ndani ya ile famille. Moya kati ya bale bazungu bawili jina yake alikuwa ni Mabi Mampanya.

Kitabu bale bazungu bali andikaka, jina yakio ni Bible noire. Sababu gani balileta ile jina? Sababu baliona asema, mambo ya bantu bale balitumika na kusungumuza nabo hayiachane kabisa na mambo ile iko mu Bible. Ndiyo maana, bali ita ile kitabu yabo asema ni Bible ya bantu beushi. Mu Bible si njo mule tuko na soma ma commandements ya Mungu na ya ba nkambo. Muko mashauri mingi sana ya kutengeneza nayo ginsi ya kuikala na bantu muzuri. Hakuna wakati ya kuingiya mu tu ma njiya tote tule ile kitabu ina fungula. Kikubua ni kujua tu asema, ba nkambo balikuwaka na mawazi ya kufanana na ile ya mu Bible. Sasa ile mambo ita kuwa ya shetani namna gani? Mabika Kalanda anapima mu kitabu yake kuonesha asema, ile mambo ya kia kuetu, ile mambo tunaita asema, ni ya ki asili ao ya ba nkambo, ni mambo ya mungu. Haiwezi kuwa mambo ya shetani hapana. Lakini mina mu lanjiyako kiloko. Njo kusema, mina exagérer kiloko mu commentaires yangu. Mabika Kalanda alipenda zaidi kuonesha asema, hautu achane mu bu muntu na bantu bengine. Alipenda tena kukumbusha asema, kuko bintu mingi sana bizuri bile ba nkambo bali tanguliaka kuona. Sasa muntu wa kutoka mbali anakuya kuelezeya bantu asema ile mambo yote ya ba nkambo ni ya bongo. Bantu bamoja banabakiya ku ile mambo ya ba nkambo. Bengine bana itshika mafundisho ya sasa. Bana kuwa banasema kama mambo ya ba nkambo ni mambo ya shetani. Mambo ya sasa, njo kusema ile mambo ya bazungu, njo mambo ya Mungu.

Sasa tunajiuliza: mambo ya Mungu inaweza kutuma muntu kukamata bengine butumuwa? Mambo ya Mungu inaweza kutuma muntu kuenda kuiba mali ya benyewe? Mambo ya Mungu inaweza kutuma muntu kwanza kukatala kupatia bantu dipanda? Ao kucheka ba nkishi ya ba nkambo ya mwenjako lakini una baleteya ba nkishi ya ba nkambo yako? Njo ile maulizo ilikuwa na bantu sa ba Simon Kimbangu. Bale bantu bote banaitaka mu bitabu asema ni ba prophètes africains ni bantu balipenda kuona wazi, kuona clair mu mambo ya mungu inyewe ile. Njo pale bengine balianza kujisomeya bobenyewe Bible. Banaona asema, kuko bintu bia mingi bile binafanana na bia ku Afrika. Njo pale balipenda kuitika Bible tena na kuitika Afrika. Hiyi mambo minatoka mukusema kua kifupi ni ile banataja mu bitabu ya bazungu na mu bitabu ya bale balifunda masomo ya bazungu asema inculturation. Mambo yenyewe ile beko bana fuata pale ni ya kusema tu asema biote bia ba nkambo habikukuya bibaya hapana. Kumbe kama ni vile tuchunge bizuri na tutupe bibaya. Lakini tuendeleshe kusema, kuimba na kupika maringa mu kia kuetu. Njo kusema tena asema inapashua kupima kuulizisha , kufanya remise en question. Ile banaita inculturation tuna weza kusema asema ni "kufuata mambo ya mungu mu mambo ya ba nkambo"

Ukumbusho 18: Kiswahili kia Katanga mu Kasai na kia Kasai mu Katanga

Ulizo ya kuanza kuanza tu pa hiyi mazungumuzo ya ukumbusho ni ya kujua kwenyewe kiswahili kia Katanga kilitokaka. tunaisha ku toucher ku iyi mambo siku moya. Lakini hayina mubaya kukumbuka tena bile tulisungumuzaka. Kama unaenda ku Katanga, hakuna kabila hata moja ile inaweza kusema kama kiswahili ni luga yayo. Bote beko tu na luga ingine pa kutoshako kiswahili. Sasa tukiende ku ngambo ya Kivu, ni namuna moja tu. Tukitambuke mayi ya tanganyka, tuna enda pale Tanzania, ni mpaka nmana iyi moja. Hiyi mifano tunaleta inataka kusema nini? Hiyi mifano inataka kusema asema, hakuna kabila hata moja pale Kongo ao pale Tanzania inaweza kusema kama hiyi luga ni yake. Kama tunasema kama hiyi luga ya swahili ni ya bantu mingi, ni kusema mara moja kama ma kabila yote ili saidiya kuakuwa ile luga inenepe na kuongeza ma mots ao ma jina ingine. Sasa ile ma mots ao ma jina itatoka wapi? Sababu gani bantu beko bana itshika hata kama haitoke mu luga ya ba nkambo yabo? Mu kiswahili ya Katanga muko ma mots ya Ciluba, ya kiluba, ya kibemba, ya ki nyasalland, ya mu fancais, ya mu lingala...Biote biko tu bienye kuchangana. Njo kusema asema bale bantu bote bana sema ile luga balifayanka ma expériences moya mu maisha na ile luga. Njo maana ile ma mots iko inasikilika kama mu kiswahili hata kama inatoka ku ngambo ingine. Njo maana banasemaka asema kiswahili ya Bukavu ni kia kuachana na kile kia Katanga. Ma expériences na kuchangana kua bantu kuna achana.

Tangu mambo ya Kyungu wa ku Mwanza ku Katanga ba Kasai mingi sana balienda ku Mbujimayi, Kananga, Kabinda, Mwene Ditu. Kama unaenda leo ku ile mikini yote, shi utan shangaa. Ni kiswahili tu pakio. Aina tu kusema asema, bantu bale balitumikaka zamani mu union-minières bana pata pension, njo bale balienda kule beko banasema kiswahili. Zamani ku Kasai balikuwaka banabacheka bantu kama banasema kiswahili. Leo iko namuna ingine. Na benye mukini na bageni, bote beko bana sema tu kiswahili. Ao tuseme aseme, benye mukini beko banashikiya. Ni kwa sababu ma taxis, na ma kazi mingi ni mpaka bale balitoka ku katanga njo bale beko nayo mu mikono. Njo kusema asema, kiswahili hakina tena mpaka ku Katanga na ku Kivu na Kisangani. Hapa sasa tunapashwa tu kusema asema kiswahili kina ingiya mu Kasai muzuri kabisa. Tena kiko na ku Kinshasa. Sababu ile wakati Kabila Mzee ali ingiya mu mukini, alianza kusema swahili ya Tanzania. Yeye shi ali ishi kule miaka mingi. Sasa ba soda yake mingi na bale alipatiya cheo, shi ni bantu balitoka naye Tanzania ao bantu bale beko nabo banasema kiswahili. Njo mu ile namna kiswahili kina ingiya mu Kinshasa. Hata ku aérport ya Njili, unaweza kusema kiswahili bote banakushikiya. Lakini kuko tena bale balikimbiya ku Katanga bana kosa kaji ku Mbujimayi ao bana shindwa namna ya ku ji intégrer kule. Bale bote shi balienda nabo ku Kinshasa. Njo mu ile namna Kiswahili kinakuja sasa luga ile presque mugini mujima iko inasema. Lakini hakuna muntu hata moja anaweza kusema kama ile luga ni yake. Exceptions ni aba batoto beko banazalikwa mu ma ville ya leo. Bababa yabo beko na sema nabo mpaka francais. Sasa batoto habajuwe tena luga ya ba nkambo yabo. Bana anza kusema mpaka francais na lingala, ao francais na kiswahili. Kiswahili kina kuya sasa njo luga ya ba nkambo yabo. Habana na luga ingine tena.

Turudiye mbele kumukongo juu ya kuendelesha mawazo moya tuliacha tu mu njiya. Ile mawazo ni ya kusema asema, kama kiswahili kina endeleya hivi ku Kinshasa na ku Kasai, kita kamata ma formes ingine kufuatirisha na ma expériences ile bantu beko bana fanya. Kiswahili kia ku Kasai kita ingisha ma mots ya ma mboka ile bantu banapenda kula kule. Tutaye ma mifano kidogo. Kule ku Mbujimayi kuko ma mboga sa "mwana kenda", "tubola mu mbadi", bitukumbana", "tusha".."Mwana kenda" ni ka kitoyo keko na eneya mu mukono ya mutoto. Pa kula bukari, kila mutoto eko anapata kake. Njo mana banakaita asema "Mwana kenda". Maana yake: kila mutoto na kake. Sasa "tubola mu mbadi" na to ni tu samaki tuloko tuko tuna anjiyaka kuoza mu mbavu yato. Tubola mbadi maana yake ni: tunaoza mu mbavu. "Bitukumbana" ni bimamboka bia shipo beyi. Bile bitaweza kunueneya mweye bote pa kuria bukari. Bitukumbana maana yake ni: bitueneye. "Tusha" ni tu samaki banaitaka mu francais asema anguilles. Sasa ma mboka ingine sa ma bitekuteku binaishaka kuingiya mu kiswahili zamani. Mu makanisa ya sasa, ma églises de réveil, muko ma luga ya kuachana. Kuko bale balitokeya ku Katanga tena balizobeleyaka kusali mu ma groupes de prières mu kiswahili. Bale banaendelesha na ile namna yabo ya kusali ata kule ku Mbujimayi. Kijana moja wa mu ile ma nkundi, alinielezeya mu kiswahili asema, pa kuanza ile ma sala yabo, banafanyaka mbele animation. Mule mu animations, njo mule eko ana mulukiya mbele mungu, anamupeluma juu ya kumuelezeya asema biote ni biake. Sasa kuko bale balizobeleyaka hata kule ku Katanga kusala mpaka mu Ciluba. Tena kuko bale bali pataka njia ya Mungu ku Amerika..bale nabo ni ba ma anglais mingi mingi tu. Sa vile bantu beko banafanya commerces kutoka Katanga kuenda Kasai na kurudi, kiswahili kita nenepa sa vile mutoni inaendaka iko inanenepa pa kupata ma mayi ya ma mitoni ya kuachana.
Kua kumueshimiya na kumupigiya baba Anna aksanti juu ya kazi ya kujulisha mambo ya pale Katanga mu dunia mujima
Baba Achille




[Ukumbusho (top of page)]

[LPCA Home Page]


© Achille Mutombo
The URL of this page is: http://www.lpca.socsci.uva.nl/aps/vol8/ukumbusho.html
Deposited at APS: 25 October 2006